Quantcast
Channel: Magazeti ya Tanzania - Tanzania Newspapers | Magazetini
Viewing all articles
Browse latest Browse all 132783

Mkenya airahisishia kazi Yanga

$
0
0
NA MICHAEL MAURUS WAPINZANI wa Yanga katika mchezo wa raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Zesco United ya Zambia, leo itashuka dimbani kucheza na Zanaco, ukiwa ni mchezo wa Ligi Kuu ya kwao, huku Wanajangwani wakizidi kurahisishiwa kazi kuelekea kipute chao. Mchezo huo wa Zesco na Zanaco ambao ni wa ufunguzi wa ligi, utapigwa kwenye Uwanja wa Levy Mwanawasa mjini Ndola, huku wapinzani hao wa Yanga wakiwa ndio wenyeji. Hivyo, leo itakuwa ni nafasi adimu kwa Yanga kuwasoma Zesco kutokana na ukweli kwamba wapinzani wao hao watalazimika kutumia mbinu zao zote kupata ushindi ili kulipa kisasi cha kufungwa mabao 4-1 na Zanaco msimu uliopita. Ukiachana na hilo, Yanga wamepata zali lingine kuelekea mchezo wao na Zesco baada ya washambuliaji wawili wa mabingwa hao wa Zambia kuchonganishwa hali itakayowafanya kutokuwa na ushirikiano unaostahili kila mmoja akisaka ufalme, hiyo ikiwa ni faida kwa kikosi cha Mwinyi Zahera. Beki wa Sofapaka ya Kenya, George Maelo ndiye ‘aliyemwaga upupu’ katika safu ya ushambuliaji ya Zesco akiwachonganisha Jesse Were na straika mpya wa timu hiyo raia wa Uganda, Umaru Kasumba. Maelo amemwabia Were kuwa Kasumba ametua Zesco inayonolewa na kocha wa zamani wa Yanga, George Lwandamina, kumaliza ufalme wake kwani Mganda huyo ni hatari kwa kucheka na nyavu. “Kasumba ni mshambuliaji hatari, naamini atamfunika Were na kumaliza ufalme wake Zesco, cha msingi ampe ushirikiano,” alisema Maelo raia wa Kenya. Were alijijengea ufalme ndani ya Zesco United akiwa kama mpachikaji wao mahiri wa mabao na kwamba Maelo anadhani mchuano wa kuwania umwamba wa kufunga baina ya washambuliaji hao, utakuwa mkali. Kutokana na hilo, ni wazi Were hatakuwa tayari kumpa ushirikiano Kasumba kuepuka kuporwa ufalme wake mbele ya mashabiki wa Zesco, hiyo ikiwa ni faida kubwa kwa timu pinzani, wakiwamo Yanga kuelekea mechi baina yao na wababe hao wa Zambia, Septemba 13, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Wakati huo huo, Yanga imetuma mashushushu mjini Ndola kwenda kushuhudia mechi kati ya Zesco na Zanaco, ikiwa ni sehemu ya kuzisoma mbinu za Lwandamina. Kiongozi mmoja wa Yanga, ameliambia BINGWA kuwa watu wao walioondoka nchini jana asubuhi, wataipeleleza Zesco katika kila idara na watakaporejea, kumkabidhi ripoti kocha wao, Zahera. “Hilo ni kweli ila siwezi kukutajia majina ya watu tuliowatuma Zambia, siku hizi mitandao imeharibu kila kitu, chochote kinachotoka kwenye vyombo vya habari, sekunde tu, kimeenea dunia nzima,” alisema kiongozi huyo ambaye hakupenda kutajwa jina. Kikosi cha Yanga baada ya kuitoa Township Rollers ya Botswana katika hatua ya awali, kinatarajiwa kujichimbia jijini Mwanza kukisuka zaidi kikosi chao tayari kumtoa nishai Lwandamina.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 132783

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>