Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, John Kerry, yupo Nairobi, Kenya, kwa ziara ya kikazi ya kudumisha amani.
Bwana Kerry atafanya mazungumzo na mawaziri wa mambo ya nje wa Afrika Mashariki juu ya namna ya kuizuia nchi ya jirani ya Sudan Kusini kutumbukia tena kwenye vita ya wenyewe kwa wenyewe.
Anategemea kukutana na rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, kabla ya kujiunga na mawaziri hao kwa mazungumzo ya namna ya kuhakikisha amani inadumishwa katika taifa hilo jipya kabisa...
↧