Quantcast
Channel: Magazeti ya Tanzania - Tanzania Newspapers | Magazetini
Viewing all articles
Browse latest Browse all 132783
↧

Mwakalebela amwibua Maximo Yanga

$
0
0
NA HUSSEIN OMAR KOCHA wa zamani wa Yanga na timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, Mbrazili Marcio Maximo, ameibuka na kuwataka wanachama wa klabu hiyo kumpigia kura mgombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti, Fredrick Mwakalebela, katika uchaguzi mkuu utakaofanyika kesho. Maximo anayejishughulisha na shughuli zake binafsi hivi sasa nchini Brazil, aliwahi kukinoa kikosi cha Yanga msimu wa mwaka 2014 chini ya uongozi wa aliyekuwa Mwenyekiti wa klabu hiyo, Yussuf Manji. Ikumbukwe wakati akikinoa kikosi cha Stars mwaka 2006 hadi 2010, Maximo aliwahi kufanya kazi na Mwakalebela kipindi hicho akiwa Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF). Akizungumza na BINGWA jana, Maximo amewatakia wanachama wa Yanga uchaguzi mwema, huku akiwasisitiza kumchagua Mwakalebela kwani utendaji wake wa kazi unafahamika kwa kila mdau wa soka hapa nchini. “Nimefurahi kusikia Yanga wanafanya uchaguzi na Mwakalebela ni miongoni mwa wagombea, naomba wanachama wafanye uamuzi sahihi kwa kuchagua viongozi sahihi,’’ alisema Maximo. Aidha, aliwasihi wanachama wa Yanga wachague watu wa mpira kwani klabu hiyo ina rasilimali nyingi za kuifanya iweze kuwa tajiri kama ilivyo TP Mazembe ya DR Congo na klabu nyingine barani Afrika. Maximo alikwenda mbali zaidi na kusema wakati alipokuwa akiinoa Yanga alitamani kuona klabu hiyo inamiliki uwanja wake na kituo cha soka, lakini ilishindikana kutokana aina ya viongozi waliokuwepo. “Nilipigania kuanzishwa kituo cha michezo ambacho kingesaidia kupatikana  wachezaji wengi vijana watakaocheza timu kubwa na pengine baadaye wangeuzwa, lakini nilishindwa,’’ alieleza Maximo. Wakati huo huo, mgombea huyo jana aliendelea kufanya kampeni na kuwataka wanachama watakaopiga kura kesho kumchagua kwani anajua kitu ambacho Wanayanga wanakitaka. “Mimi sina mengi ila nipewe nafasi nifanye kwa vitendo, naomba wanachama wote wa Yanga waliopo mikoani na kwingineko wajitokeze kwa wingi kesho wapige kura za ndiyo kwangu,’’ alisema Mwakalebela.
↧

Viewing all articles
Browse latest Browse all 132783

Latest Images

Trending Articles

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>