Quantcast
Channel: Magazeti ya Tanzania - Tanzania Newspapers | Magazetini
Viewing all articles
Browse latest Browse all 132783

Tiboroha: Mabadiliko Yanga lazima

$
0
0
NA ZAITUNI KIBWANA MGOMBEA wa nafasi ya mwenyekiti katika uchaguzi mkuu wa Yanga, Dk. Jonas Tiboroha, amesema ana sera sita alizozigawanya makundi matatu lakini kubwa ni kufanya mabadiliko ndani ya klabu hiyo. Tiboroha ni miongoni mwa wagombea watatu waliobaki kuwania nafasi ya mwenyekiti katika kinyang’anyiro hicho baada ya kujitoa kwa Elias Mwanjala aliyedai ana majukumu mengi. Akizungumza na BINGWA jana, Tiboroha alisema, ili Yanga iweze kushindana na klabu kubwa ni lazima ifanye mabadiliko ya mfumo. “Ni lazima Yanga ibadili mfumo iwapo inataka kushindana na klabu kubwa barani Afrika kama TP Mazembe na timu nyingine zenye mafanikio. “Si vibaya kuiga mambo mazuri kama walivyofanya Simba, sisi tulikuwa waasisi wa mabadiliko kipindi cha Mwenyekiti, Abbas Tarimba, lakini hatukufanikiwa na sasa tunataka kurudia sera hiyo,” alisema. Aidha, alisema mbali na mabadiliko ya muundo pia sera yake ni kuwaunganisha Wanayanga kuwa kitu kimoja ili kuondoa tofauti zao. “Hii ni timu ya wananchi, tutaanza kuongeza mashabiki mpaka wanachama ili kuwaweka karibu na timu yao,” alieleza Tiboroha. Pia alisisitiza jambo jingine kuwa ni kuandaa mpango wa muda mfupi ambao utaleta tija kwa manufaa ya klabu hiyo wakati wakijiandaa kubadilisha mfumo

Viewing all articles
Browse latest Browse all 132783

Latest Images

Trending Articles

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>