Quantcast
Channel: Magazeti ya Tanzania - Tanzania Newspapers | Magazetini
Viewing all articles
Browse latest Browse all 132783

Shonza mgeni rasmi siku ya urembo wa asili

$
0
0
NA BRIGHITER MASAKI NAIBU Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza, anatarajia kuwa mgeni rasmi katika onyesho la Siku ya Urembo wa Asili Tanzania, linaloanza leo na kuendelea kesho katika ukumbi wa Life Park, Mwenge, Dar es Salaam. Akizungumza na BINGWA jana, mwandaaji wa onyesho hilo, Antu Mandoza, alisema yatatolewa mafunzo ya kutengeneza vipodozi vya asili visivyo na kemikali bure na  kutakuwa na upimaji saratani ya matiti na elimu ya saratani mbalimbali bila malipo. “Kutakuwa na kipaumbele kwa wanawake wajasiriamali wa kundi maalumu kama vile walemavu kushiriki katika maonyesho haya  ambapo watapewa banda bure la kuonyesha kazi zao pamoja na wajasiriamali vijana,” alisema Antu. Katika burudani, wasanii kama Khadija Kopa, Aneth Kushaba, Mwasiti, Grace Matata, huku Rose Ndauka, mchekeshaji Jaymond na mtangazaji Dina Marious  watazungumza na watu.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 132783

Latest Images

Trending Articles

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>