Quantcast
Channel: Magazeti ya Tanzania - Tanzania Newspapers | Magazetini
Viewing all articles
Browse latest Browse all 132783

Aussems acharuka Simba

$
0
0
NA WINFRIDA MTOI LICHA ya kuanza Ligi Kuu Tanzania Bara kwa ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya JKT Tanzania, Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Aussems, bado anaumiza kichwa juu ya kikosi chake. Simba iliibuka na ushindi huo katika mechi iliyopigwa juzi kwenye Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam. Katika mchezo huo, Aussems alibadilisha kikosi chake tofauti na kile kilichoonekana michezo miwili ya Ligi ya Mabingwa Afrika na Ngao ya Jamii walipokutana na Azam FC na kuibuka kidedea, wakishinda mabao 4-2. Moja ya sababu iliyomfanya Aussems kubadili kikosi ni kutokana na baadhi ya nyota wake kama Shomari Kapombe, John Bocco na Pascal Wawa kuwa majeruhi, huku Jonas Mkude akisumbuliwa na homa. Wekundu wa Msimbazi hao walianza ligi wakiwa tayari wameondolewa katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na UD Songo ya Msumbiji iliyosonga mbele kwa faida ya bao la ugenini baada ya kutokana sare ya 1-1, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, mechi ya awali wakitoka suluhu nchini kwao. Kitendo hicho kiliwafanya Simba kupania ligi kuu kwa sababu ndiyo michuano pekee itakayowarudishia heshima yao endapo watafanya vizuri na kutetea ubingwa wao. Kutokana na hilo, matarajio ya benchi la ufundi ilikuwa ni kuanza kwa ushindi wa mabao mengi zaidi ya matatu waliyoifunga JKT Tanzania. Kauli ya Aussems baada ya mechi hiyo ilidhihirisha kuwa lengo lake halijatimia kwa kusema walistahili kushinda mabao mengi zaidi ya 3-1. Kocha huyo aliweka bayana kutoridhishwa na matokeo na uchezaji wa nyota wake kwa kile alichodai dakika za mwisho, walionekana wakicheza kama watoto. “Katika mchezo huu tulitakiwa kushinda mabao mengi zaidi, sijaridhika kwa nafasi na kikosi nilichopanga, tulitakiwa kufunga mabao manne hadi sita, ila kuna makosa na dakika 15 za mwisho tulicheza kama watoto,” alisema. Alieleza kuwa kuelekea mechi zijazo, ataendelea kuwandaa wachezaji wake kisaikolojia ili kusahau matokeo yaliyopita ya kutolewa katika michuano ya kimataifa, akiamini itasaidia kufanya kile anachohitaji.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 132783

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>