NA SISCA MACHABA (TUDARCo)
MWIGIZAJI nyota wa tamthiliya ya
Rebecca, Wellu Sengo, amewatangazia mashabiki kuwa amebadili dini kutoka
Ukristo na kuingia Uislamu, uamuzi utakaokwenda sambamba na kubadili jina lake.
Mrembo huyo mwenye umbo matata ambaye
pia ni mzazi mwenza wa Steve Nyerere, alitumia ukurasa wake wa Instagram kutoa
taarifa hiyo, akisema: “Assalamu Allaykum, leo tarehe 29 Agosti 2019, mimi
Wellu J Sengo nimeslimu na kuwa Amina J Sengo, naombeni ndugu zangu katika imani
mnishike mkono.”
↧