Washington.Wayne Rooney ametua Washington, Marekani kwa ajili ya kukamilisha mazingumzo na kufanya vipimo leo Alhamisi kuhusu uhamisho wake kutoka Everton kwenda DC United.
Jana, Rooney alikatisha mapumziko mafupi aliyokuwa pamoja na familia yake ndani ya Barbados ili kukamilisha mpango wake huo wa baadaye.
Rooney alikuwa katika Visiwa vya Caribbean tangu wiki iliyopita. Kwa sasa atakuwa akizungumzia kiasi cha Pauni 300,000 kwa wiki kutoka katika klabu hiyo mpango huo ukikamilika leo.
↧