Shirika la utafiti wa anga za juu (Nasa) Jumapili lilizindua chombo cha uchunguzi ambacho kitarushwa na kuzunguka karibu zaidi na jua kuliko chombo kingine chochote kilichowahi kutumwa.
↧
Nasa wazindua chombo kwenda ‘kugusa jua’
↧
Mkuu wa Wilaya kushuhudia 'Papasa Square' ya Ruvu Shooting
Ruvu Shooting imepanga kutumia mchezo huo wa kirafiki kama sehemu ya utambulisho wa mfumo wao mpya wa 'Papasa Square'.
↧
↧
Kikosi cha Malkia Strikers kinachoenda Japan hadharani
Katika kikosi hicho kilichosheheni nyota kibao akiwemo Nahodha Mercy Moim, Trizah Atuka na Jane Wacu, Munala amewajumuisha wachezaji wawili wapya ambao ni Lorine Chebet na Sharom Chepchumba
↧
Kerr: Ratiba hii inachosha, KPL legezeni kidogo
Kauli ya Kerr imekuja wakati ambapo kwa mujibu wa msimamo ulivyo hivi sasa, mabingwa hao mara 16 wa KPL, ambao wanaongoza msimamo wakiwa na pointi 60 kileleni, mechi tatu mkononi huku wakiwazidi wapinzani wao wa Karibu Bandari FC kwa jumla ya pointi 12.
↧
Samuel Eto’o atua Qatar
Mshambuliaji wa zamani wa Barcelona, Inter Milan na Chelsea, Samuel Eto’o, anakamilisha taratibu za kujiunga katika Ligi Kuu ya Qatar kukipiga katika klabu ya Qatar Sports Club ya Ligi Kuu.
↧
↧
Murray ang’oka Cincinnati Masters
Cincinnati, Marekani. Mchezaji namba moja wa zamani kwa ubora wa tenisi duniani, na namba moja nchini Uingereza kwa sasa, Andy Murray ameshindwa kufurukuta baada ya kutolewa na Lucas Pouille wa Ufaransa, katika raundi ya kwanza ya mashindano ya Cincinnati Masters.
↧
Dina atwaa medali tatu za dhahabu
Mchezaji Dina Asher-Smith amejiandikia historia kwa kutwaa medali tatu ya dhahabu kwenye mashindano ya Ulaya ‘European Championships’ akiiongoza Uingereza kushinda mbio za kupokezana vijiti za mita 4x100, mjini Berlin, Ujerumani.
↧
Martinez, Thierry Henry wanukia Leicester City
Uongozi wa klabu ya Leicester City, unafikiria kulifumua benchi lake la ufundi na kuingiza sura mpya huku Kocha wa timu ya Taifa ya Ubelgiji, Roberto Martinez na msaidizi wake Thierry Henry wakitajwa kumrithi Claude Puel.
↧
David Silva atundika daluga Hispania
Manchester, England. Kiungo wa Manchester City, David Silva, ametangaza kustaafu kuitumikia timu ya Taifa ya Hispania, baada ya kuitumikia mfululizo kwa miaka 12.
↧
↧
Wadau waweka kiulizo Harambee stars itakayoivaa Ghana
Migne amewaita nyota 18 wa ndani na maproo 19 waliokuwa wanakipiga katika vilabu mbalimbali nje ya nchi
↧
Tanzeela Qambrani: Mwanamke mwenye asili ya Tanzania ateuliwa mbunge Pakistan na kuweka historia
Tanzeela Qambrani, kutoka jamii ndogo ya Sidi mababu zake walitokea nchini Tanzania na ndiye mbunge wa kwanza mwenye asili ya Afrika.
↧
TUENDAKO: ABSALOM KIBANDANI ACHAMBUA FIFRA ZA SHIVJI, MAARIFA YA ZITTO KWA CCM NA JPM
Na Absalom Kibanda |
NIANZE mapema kukiri kwamba ninao udhaifu mkubwa kifikra, ambao kwa kiwango kikubwa ndio umekuwa mwongozo wa tafakuri zangu kwa takribani miaka 26 sasa.
Udhaifu huo si mwingine bali ni ujinga wangu wa kuamini kwamba msingi wa hoja zangu kila ninapoangalia mustakabali wa kiuongozi na hatima ya taifa letu, unapaswa kuakisi fikra za wanafalsafa mahiri wawili, Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere na Profesa (mstaafu) wa sheria, Issa Shivji.
Yumkini, wasomaji wa maandishi yangu ambao kinara miongoni mwao ni mimi mwenyewe, watakubaliana nami kwamba udhaifu wangu wa kurejea fikra za wanazuoni hao wawili, hauko katika misingi ya ukasuku wa kukubaliana au kupinga chochote ambacho ama waliwahi kukisema au kukiandika.
Nimeanza na kukiri udhaifu huo ili kupata uhalali wa kurejea tena juu ya kile ambacho kilipatwa kusemwa na Profesa Shivji miaka 26 iliyopita, wakati taifa lilipokuwa ndio kwanza linajiandaa kurejea katika mfumo wa siasa na demokrasia ya vyama vingi.
Nilikuwa mwanafunzi wa Shahada ya Kwanza katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) katika kipindi cha kati ya mwaka 1991/92, wakati Profesa Shivji aliposimama ndani ya ukumbi maarufu wa Nkrumah na kutoa maoni yake juu ya aina ya siasa ambayo taifa letu lilipaswa kuchukua.
Hicho kilikuwa ndicho kipindi ambacho dunia ilishuhudia kuibuka kwa fikra mpya za wakati huo, zilizokwenda sambamba na kumalizika kwa vuguvugu la miaka takribani 70 ya vita baridi ambavyo viliigawa dunia katika pande kuu mbili – Mashariki na Magharibi.
Vuguvugu hilo ndilo ambalo hapa nchini lilichagizwa na uamuzi wa Rais Ali Hassan Mwinyi, kuunda tume iliyokuwa ikiongozwa na aliyekuwa Jaji Mkuu wa Tanzania wakati huo, Jaji Francis Nyalali na kukusanya maoni ya Watanzania juu ya aina ya mfumo wa siasa wa ama kuendelea na chama kimoja au kurejesha vyama vingi.
Tume hiyo ilipofika Mlimani, mwanazuoni ambaye maoni yake yaliibua kishindo kikubwa cha hamasa na ushabiki wa zama zile za ‘mapinduzi ya fikra’ alikuwa ni Profesa Shivji, ambaye alitumia muda wa kutosha kueleza mawazo yake.
Akizungumza kwa umakini na ufasaha, Profesa Shivji ambaye hakuna shaka kwamba ndiye aliyekuwa mwanazuoni maarufu zaidi chuoni hapo wakati huo, alisema changamoto kubwa ya kuukubali mfumo wa vyama vingi hapa nchini ni sura halisi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Profesa Shivji aliiambia hadhara iliyojaa Nkrumah siku hiyo, kwamba CCM haikuwa ni chama cha siasa bali kwa historia yake na kwa mizizi ya kiuongozi na kiutawala iliyojijengea, ilikuwa na taswira ya kuwa chama dola zaidi.
Hakuishia hapo, bali alikwenda mbele na kueleza iwapo kweli taifa lilikuwa linataka mfumo thabiti na halisi wa demokrasia ya vyama vingi, basi taswira hiyo ya CCM ya chama-dola, ilipaswa ‘kufa’ kwanza kabla ya kuruhusu vyama shindani vya siasa kuchuana katika uwanja tambarare (level playing field).
Wakati ukumbi ukiwa umetulia kumsikiliza, Profesa Shivji aliwageukia wasomi na wanasiasa na kusema wasomi wa aina yake walikuwa ni watu waliokuwa wakipenda kuchambua masuala ya siasa kisomi na kwa uhuru, tofauti na wanasiasa ambao kwao mwelekeo wowote wa fikra miongoni mwao hitimisho lao lilikuwa ni kusaka fursa za madaraka.
Kwa maneno yake mwenyewe Shivji alisema; “Wasomi wanapenda siasa, hawapendi madaraka, wanasiasa hawapendi siasa wanapenda madaraka.” Mvumo wa shangwe, kelele na makofi ulisikika bayana masikioni mwa umati mkubwa wa jumuiya ya wana Mlimani wa zama hizo waliokuwa ukumbini mle.
Tume ya Jaji Nyalali ilipomaliza kukusanya maoni na Sheria ya Vyama Vingi ikapitishwa rasmi Julai 1992, CCM – dola ilibakia na taswira ile ile, hali ambayo imeendelea kubakia ile ile.
Ni miaka 26 sasa tangu Profesa Shivji alipoyasema maneno hayo, ambayo kila siku inayosonga mbele, uhalisi wake katika medani ya siasa za Tanzania na hususani katika uongozi wa taifa letu unazidi kuakisi kile alichokisema.
Ndani ya mfumo wa vyama vingi, CCM ya leo inazidi kujizatiti kidola pengine kuliko wakati mwingine wowote tangu mfumo wa vyama vingi uanze.
Ni juzi tu hapa Rais Dk. John Magufuli, mkuu wa nchi ambaye sina shaka hata kuandika kwamba huko tuendako baada ya kuhitimisha urais wake ataacha alama nyingi zitakazoumiza na kukuna vichwa wanazuoni, alitamka bila kuuma maneno kwamba CCM ndiyo mhimili wa uongozi wa taifa.
Huku akiwataja kwa majina na nyadhifa zao wasaidizi wake wakuu, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu kuwa wote ni wana CCM jambo ambalo ni kweli, JPM kwa kauli thabiti alikwenda mbele na kusema hadharani kwamba hata Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi eti naye alikuwa mwana CCM.
Haikuwa mara ya kwanza, ya pili au ya tatu kwa Rais Magufuli ambaye yeye mwenyewe hupenda kujiita ‘Msema kweli’, kutanabahisha hilo la CCM kwa kauli na mara kadhaa kwa vitendo vilivyo bayana.
Ni Rais Magufuli yeye mwenyewe ambaye katika moja ya kauli zake kwa wakurugenzi wa wilaya, miji na majiji, alipata kutoa kauli ya kueleza kushangaa kwake iwapo atatokea mmoja wapo akatangaza matokeo ya uchaguzi utakaompa ushindi mwanasiasa ambaye si mwana CCM ilhali akijua ameshika wadhifa huo kwa uteuzi uliofanywa na Mwenyekiti wa Taifa wa CCM.
Kauli zenye mwelekeo huo za JPM ambaye sina shaka kumwelezea kuwa ni mmoja wa marais madhubuti kutokea hapa nchini na pengine Afrika, si tu kwamba zinarejea tafakuri ya miaka 26 ya Profesa Shivji juu ya udola-dola wa CCM, bali zinaibua pia shaka iwapo washauri wa Rais huwa wanapata muda wa kutosha kutafakari kwa kina athari na pengine maana halisi ya kile ambacho kiongozi huyo anakisema na kukifanya akiwa mkuu wa nchi.
Ingawa JPM ninayemjua kwa miaka mingi ni kiongozi mkali kwa hulka, asiye na masihara katika kazi tangu nilipomfahamu akiwa naibu waziri zaidi ya miaka 20 iliyopita, kwa nafasi ya juu kitaifa aliyoishika sasa, anapaswa kuwa na washauri wa masuala ya siasa wa aina au wa kiwango cha profesa, ambao watachagiza kumwongezea umakini na pengine umahiri wakati anapotekeleza wajibu wake.
JPM huyu si yule tena waziri ambaye baadhi yetu tulikuwa huru kuingia katika ofisi yake akiwa ofisini na kueleza kwa maana ya kupambana naye kwa hoja na kifikra juu ya namna mambo yalivyokuwa yakienda ndani ya wizara alizopata kuziongoza.
JPM huyu wa leo ni Rais ambaye naamini baada ya kukaa Ikulu akiwa Amiri Jeshi Mkuu, mkuu wa nchi na kwa sehemu ndogo Mwenyekiti wa Taifa wa CCM, sasa anatambua kwamba swali lake au maoni tu vinatosha kuonekana, ikatafsiriwa na ikafanyiwa kazi kama amri halali.
Ni rahisi leo kwa mchambuzi wa aina yangu kufikia hitimisho kirahisi – rahisi na pengine kwa makosa, kwamba kile kinachotokea leo hii mitaani, ambako tunaona askari polisi wakiwa na jeuri isiyomithilika ya kumkamata yeyote, wakati wowote na popote na kufanya lolote pasipo kujali chochote, ni matokeo ya tafsiri potofu za kauli za ki-maelekezo zilizopata kutolewa na wakuu mbalimbali akiwamo Rais.
Ingawa si busara na kimsingi ni jambo la aibu kubwa kuwa na jeshi lenye askari dhaifu na wasiojiamini, lakini ni fedheha kwa taifa lililojengwa na kulelewa katika misingi ya kuheshimu sheria na kutambua haki za raia, kuwa na polisi wababe wasiosikia la mtu, ambao kwa sababu tu ya kuwa na dhamana ya kulinda usalama, wako tayari pasipo kujali kupiga na kuumiza watu wasio na hatia.
Ukatili unaofanywa na baadhi ya polisi katika siku na miaka ya karibuni na ambao kwa bahati mbaya umeshindwa kukemewa hadharani si tu na wakuu wa jeshi hilo, bali pia hata na Amiri Jeshi Mkuu JPM ambaye amekuwa mwepesi sana kufuatilia taarifa mbalimbali za namna hiyo na kuzitolea kauli za kimamlaka, kwa kiwango kikubwa unaongeza shaka juu kule ambako taifa linaelekea.
Katika mazingira ambayo CCM inajitanabahisha na dola, si rahisi leo hii kumsikia kiongozi wa juu wa chama hicho tawala akitoa kauli yenye mamlaka ya kuwataka polisi kuheshimu haki za msingi za raia, kuwalinda na kutenda haki.
Unapomsikiliza Katibu Mkuu wa CCM, mwanasiasa msomi, Dk. Bashiru Ally na kumuona akitoa kauli za kuhofia kukemea matendo yasiyostahili na ya kikatili ya polisi, hupati shida kubaini ukweli kwamba hekima za kiongozi huyo zimezongwa na kivuli cha kumtaka mkuu wa nchi ndiye awe wa kwanza kuonyesha njia.
Katika mazingira ambayo sehemu mbalimbali nchini hivi sasa watuhumiwa vinara wa uhalifu ni viongozi na makada wengi zaidi wa vyama vya siasa vya upinzani, ni rahisi kwa baadhi yetu kujiuliza, matukio ya namna hii ni ya bahati mbaya au ya kupangwa.
Ni jambo lisiloingia akilini kwa Jeshi la Polisi kutaka kuliaminisha taifa leo hii, kwamba ndani ya vyama vya siasa vya upinzani na si CCM, ndiko kuliko hasa na wavunja sheria za nchi na wachochezi wanaopaswa kudhibitiwa kwa mkono wa dola kwa namna inavyoendelea sasa.
Limekuwa ni jambo la kawaida sasa, kuona na kusikia baadhi ya wabunge au madiwani wanaotokana na vyama vya upinzani, kuburutwa na polisi kwa namna ya kudhalilika na isiyo na staha, ambayo kwa baadhi yetu ukakasi wake haupaswi kuishia katika kulalamika na kulaani tu bali kuchukuliwa kwa hatua madhubuti.
Taifa limeshuhudia kumalizika kwa kampeni na uchaguzi mdogo wa madiwani na wabunge katika maeneo mbalimbali nchini.
Kile kilichotokea Tarime kwa mfano wakati wa mikutano ya kampeni ya udiwani, ambako Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko (Chadema) alikamatwa na kusemekana kupigwa na polisi, ni mfano mmojawapo wa matukio ya namna hii ambayo kwangu yanalifedhehesha taifa.
Pengine ni matukio ya aina hii ambayo yamechagiza andiko la Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT- Wazalendo), ambaye alikuwa eneo la tukio wakati Esther akikamatwa na polisi, akitaka kutafutwa kwa kile alichokiita haja ya kutafutwa kwa ‘maridhiano ya kisiasa’.
Katika sehemu moja ya andiko lake hilo lenye sehemu kuu tatu, Zitto ambaye anapendekeza kuundwa kwa Tume Huru ya Uchunguzi kwa matukio mengine kadhaa ambayo nachelea kuyataja kwa leo kwani si sehemu ya muktadha wa makala yangu, analigusa Jeshi la Polisi.
Kwa maneno yake mwenyewe, mwanasiasa huyo kijana ambaye mara kadhaa ameikosoa Serikali ya JPM kwa kukosa maarifa anaandika; “…Yafanyike mabadiliko makubwa ya Jeshi la Polisi ili kulifanya kuwa linatoa huduma ya kulinda raia badala ya kutesa raia (Polisi Service badala ya Police Force).”
Ninao uhakika wa asilimia 100 kwamba matamshi na maandishi kadhaa ya Zitto kwa Serikali, yakiwamo yale ya msingi, yamekuwa na ukakasi mwingi ambao unaonekana bayana katika majibu ya kejeli, dhihaka na dharau kutoka ama kwa viongozi wa Serikali, msemaji wa CCM au makundi mahususi ya propaganda yaliyoibuka zama hizi, yakihusisha kampeni za mitandaoni na katika magazeti.
Pengine niliseme hili mapema kwamba ziko nyakati tena mara nyingi tu, Zitto mwenyewe amekuwa mwepesi na pengine kinara wa maandishi na kauli za dharau, dhihaka, kejeli na za kuudhi dhidi ya viongozi, Serikali na hata CCM.
Mwenendo huo wa hovyo wa Zitto, wakati mwingine unaweza ukafanana na mara kadhaa kubeba ujumbe ule ule wa makundi kadhaa ya propaganda yaliyoibuka zama hizi, yakipigia chapuo yale wanayoyaona kuwa ni mafanikio ya mfano na kujivunia ya Serikali ya JPM. Haya yanahitaji mjadala mahususi.
Hata hivyo, makosa au upungufu huo wa kibinadamu wa Zitto kama ulivyo kwa viongozi wengine wa kisiasa walioko ndani na nje ya Serikali, hayafuti ukweli wa kile ambacho mara kadhaa mwanasiasa huyo kijana jasiri amekuwa akikibeba nyuma ya msamiati wake mama wa sasa, ‘maarifa’.
Kwa muktadha wa andiko langu la leo, maarifa ambayo taifa tumeyakosa leo, ni kushindwa kwetu kuchukua hatua madhubuti na makini za kuliondoa taifa katika mkondo wa CCM kuendelea kuwa chama dola badala ya kuwa chama kilicho madarakani.
Kwamba Rais wa nchi, Katibu Mkuu wa CCM na Mwenyekiti kukifungamanisha chama na Serikali katika falsafa zao za kiuongozi na katika uamuzi na mwelekeo wa jumla wa kitaifa, hilo peke yake ni tatizo.
Katika mazingira ambayo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi anapata jeuri na anaachwa tu aendelee pasipo kukemewa hadharani, kutembea na kuitangaza Ilani ya CCM kwa wakuu wa vyombo vya usalama vilivyo chini ya mamlaka yake kwa namna ile ile ilivyofanywa wakati wa mfumo wa chama kimoja, ni rahisi sana kujua ukubwa wa tatizo hili kifikra.
Katika mazingira ya namna hii, wala sipati shida ninapoona msamiati ‘haki’ ukiwa adimu midomoni mwa viongozi takriban wote wa juu, ambao ama wanashiriki au kuchagiza kuteuliwa kwa makada kindakindaki wa CCM katika nafasi za utumishi wa umma kama za ukurugenzi wa majiji, manispaa, miji na wilaya.
Hivi unatarajia nini kitafanyika au kutokea wakati wa uchaguzi wa udiwani, ubunge na hata urais utakapofanyika huku wakurugenzi hao ndio huwa wasimamizi wa uchaguzi kwa niaba ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)?
Ni jambo la bahati mbaya kwamba katika mkutano wake wa juzi na waandishi wa habari, Dk. Bashiru, mmoja wa wachambuzi mahiri wa masuala ya siasa na uongozi zama akiwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na ‘mwanafunzi’ wa fikra za Profesa Shivji hakuulizwa swali hilo.
Nitakuwa sijakosea iwapo nitahitimisha andiko langu nikiwa na kihoro kilichowekwa kiporo kwa miaka 26 sasa cha fikra za Profesa wa Kigoda cha Mwalimu Nyerere, Shivji na chagizo la maarifa ya maudhi la mwanasiasa mwenye ushawishi, mtukutu na mahiri, Zitto kwa Serikali ya JPM na CCM yake.
↧
UCHAGUZI MDOGO NA MUSTAKABALI WA MORALI YA WAPIGA KURA
Na ANDREW MSECHU |
IMEKUWA kawaida kusikia diwani au mbunge amejiuzulu nafasi yake. Hatua hiyo ni safari mpya kuelekea kwenye uchaguzi mdogo. Wabunge na madiwani wanajiuzulu katika nafasi zao kwa sababu mbalimbali.
Alipojiuzulu ubunge na nyadhifa zake zote ndani ya CCM, aliyekuwa Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu alisema amechukua uamuzi huo kutokana na kutoridhishwa na mwendo wa siasa nchini Tanzania, ukiukwaji wa haki za binaadamu, ongezeko la vitendo vya kidhalimu dhidi ya raia na kutokuwapo kwa mipaka baina ya mihimili ya dola, yaani Serikali, Bunge na Mahakama.
Ilitafsiriwa kwamba alichukua uamuzi huo baada ya kushuhudia yaliyompata mbunge mwenzake, Tundu lissu (Singida Mashariki-Chadema) aliyekuwa ameshambuliwa kwa risasi na sasa anaendelea na matibabu nchini Ubelgiji kwa mwaka mzima sasa.
Baada ya Nyalandu, lilifuata wimbi la kujiuzulu kwa madiwani na wabunge wengine kutoka Chadema na kuhamia CCM, sababu zao kwa ujumla wao, walieleza kuwa ni kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano kutokana na utendaji wake.
Muda mfupi baadaye, Mbunge wa Siha, Dk Godwin Mollel (Chadema) na mbunge wa Kinondoni, Maulid Mtulia (CUF) walitangaza kujiuzulu nafasi zao, ikiwa ni mwendelezo wa wimbi la zaidi ya madiwani 23 wa Chadema kujiuzulu na kurejea CCM.
Wiki hii, wabunge wawili wametangaza kujiuzulu nafasi zao hawa ni aliyekuwa Mbunge wa Ukonga (Chadema) Mwita Waitara na aliyekuwa Mbunge wa Monduli (Chadema) Julius Kalanga na kuongeza idadi ya majimbo yanayotakiwa kurudia uchaguzi.
Hili linafanyia wakati kampeni za marudio ya uchaguzi zikiendelea katika kata 76 kote nchini kwa sababu tu madiwani wa kata hizo walijiuzulu nyadhifa zao kisha kuteuliwa na chama kipya walichohamia, CCM kuwania nafasi hizo hizo ambazo walijiuzulu awali.
Mengi yamefuata, mengi yameendelea kushuhudiwa, lakini zaidi ni hatua ya wananchi kulazimika kurejea katika uchaguzi wa marudio ambazo zimekuwa na gharama ya fedha, muda na morali.
Veronica Charles, mkazi wa Kinondoni alisema yeye ni mwanachama wa CCM lakini kwake yeye, marudio ya uchaguzi yaliyofanyika jimboni kwake Februari mwaka huu hayakuwa na maana tena kwake na hakuona sababu ya kupoteza muda wake kushiriki katika uchaguzi mwingine.
Alisema hata kama aliyekuwa akiwania nafasi hiyo alitokea katika chama cha upinzani na kuwania kupitia chama ambacho yeye ni mfuasi, hakuona mantiki ya kupotea muda wake kupiga kura kwa mara nyingine, wakati ingewezekana tu muhusika akajiuzulu muda mfupi kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2020 na kuwania kupitia chama hicho katika uchaguzi huo.
“Nilishiriki kikamilifu katika uchaguzi uliopita wa 2015. Ni kweli aliyekuwa mgombea wa chama changu CCM alishindwa. Maisha yaliendelea, lakini huyu mbunge hadi alipojiuzulu na kurudia uchaguzi sikuwahi kuona mkate mezani kwangu, sasa kwanini nipoteze muda wangu kwenye kampeni hadi uchaguzi mwingine wakati sjui hata wanangu watakula nini?” alisema.
Rai ya Veronica ni sehemu ya kile wanachozungumza wananchi wengi wanaopelekwa katika uchaguzi mdogo katika maeneo mengi na inaonesha taswira halisi ya mapokeo ya wananchi ambao ndio wapiga kura, kuhusu kushuka kwa morali ya kushiriki katika uchaguzi wa mara kwa mara hivyo kupunguza idadi ya wapiga kura wanaojitokeza katika uchaguzi mdogo.
Tume ya Uchaguzi
Katika uchaguzi zilizorudiwa kwenye majimbo yote matatu, yaani katika Jimbo la Singida Kaskazini, Jimbo la Siha na Jimbo la Kinondoni na katika Kata 23 ambazo madiwani wake walijiuzulu, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imekiri kwamba idadi ya wapiga kura imeshuka katika uchaguzi huo.
Katika taarifa yake ya baada ya uchaguzi mdogo wa madiwani Oktoba mwaka jana na uchaguzi mdogo wa wabunge Februari mwaka huu, NEC inasema kweli wameshuhudia mwitikio mdogo wa wananchi kujitokeza kupiga kura tofauti na idadi ya watu waliojiandikisha.
Ufafanuzi wa NEC unaeleza kuwa hiyo inatokana na idadi ya wapiga kura waliojitokeza katika uchaguzi mdogo wa ubunge wa Kinondoni na Siha uliofanyika Februari 17 pamoja na uchaguzi mwingine wa ubunge na udiwani.
Katika Jimbo la Kinondoni kati ya wapiga kura 264,066 waliojiandikisha ni wapiga kura 45,454 tu waliofika kupiga kura, hivyo wapiga kura 218,612 kutojitokeza kabisa katika upigaji kura huo.
Katika Jimbo la Siha, ilieleza kuwa kati ya wapiga kura 55,313 waliojiandikisha waliopiga kura ni 32,277 hivyo wapiga kura 23,036 kutojitokeza kupiga kura.
Takwimu zinaonesha kuwa katika uchaguzi mdogo zilizowahi kufanyika miaka ya nyuma pia wapiga kura wamekuwa wakishindwa kushiriki kikamilifu kutokana na sababu mbalimbali lakini zaidi kutokana na nia ya wale wanaojiondoa kwenye nafasi zao baada ya kuaminiwa katika uchaguzi wa awali na kurudi kuwania nafasi hizo hizo kupitia vyama vingine kupitia chaguzi ndogo.
Kwa miaka iliyopita, takwimu zinaonesha kuwa uchaguzi mdogo zilizowahi kufanyika katika majimbo ya Kalenga na Chalinze Machi 16, 2014, kati ya waliojiandikisha kupiga kura 71,964 ni 29,541 tu walijitokeza kupiga kura huku Chalinze kati ya 92,000 walioandikishwa waliopiga kura walikuwa 24,422.
Pia, Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 ni wapiga kura milioni nane pekee waliopiga kura kati ya milioni 21 waliojiandikisha huku mwaka 2015, kati ya wapiga kura milioni 23.2 walioandikishwa na waliojitokeza kupiga kura walikuwa milioni 15.6.
Hata hivyo, Naibu Katibu Uendeshaji Uchaguzi wa NEC, Irene Kadushi amewahi kukaririwa akisema mwitikio wa wapiga kura wakati wa uchaguzi mdogo hutofautiana na wakati wa uchaguzi mkuu na kitendo cha watu kuhama chama kimoja na kisha kuruhusiwa kugombea nafasi ile ile imechangia idadi ndogo ya wapiga kura kwenye uchaguzi mdogo wa Februari 17.
“Miaka ya nyuma tulikuwa na changamoto ya fedha katika kutoa elimu ya mpiga kura, lakini tatizo hilo limepatiwa ufumbuzi wa kutosha na sasa elimu ya mpiga kura ni endelevu. Hakuna taasisi yoyote inayoiingilia NEC katika utendaji wake ikiwamo Serikali ambayo jukumu lake huishia kwenye kuipatia tume fedha kwa ajili ya shughuli zake,” alisema.
Bosi huyo wa uchaguzi wa NEC alisema muundo wa tume hiyo unachangia wananchi kuwa na mtazamo kuwa wateule wa Serikali wanaosimamia uchaguzi kwenye ngazi za chini wanakipendelea chama tawala.
“Hii imepelekea (sababisha) sisi kuomba tupatiwe ofisi kwenye kanda mbalimbali hapa nchini jambo litakalotusaidia pia katika utunzaji wa vifaa vyetu vya kazi. Pia, tunataka tuwe na uwezo wa kuajiri wafanyakazi hasa wasimamizi wa uchaguzi hali itakayoiongezea tume kuaminika kwake,” alisema.
Anaonesha kwamba iwapo hilo litafanyika, litasaidia watu kuongeza uaminifu wao kwa tume ambayo imekuwa ikifanya kazi kubwa, kwani hata nchi ambazo tume zake zinaonekana ziko huru na haki bado zinalalamikiwa kwa mambo kadhaa.
Gazeti moja la kila siku (si MTANZANIA) linaikariri NEC ikieleza kwamba uchaguzi mdogo wa madiwani na wabunge ambazo zimekuwa zikifanyika kutokana na wawakilishi hao wa wananchi kufariki dunia au kuhama vyama vyao zitakoma miezi 12 kabla ya Uchaguzi Mkuu ujao.
Kauli hii inatolewa huku kukiwa na taarifa ya wimbi kubwa zaidi kuwakumba madiwani na wabunge kutoka katika kambi ya upinzani kuhamia CCM na hivyo kuwapo kwa uwezekano wa kuitishwa kwa uchaguzi mdogo ndani ya muda mfupi kila unapomalizika uchaguzi mdogo.
↧
↧
UNG’ANG’ANIZI WA BIYA NA ‘KUFELI’ KWA SIASA CAMEROON
JOSEPH HIZA, DAR ES SALAAM |
CAMEROON ni Taifa lisilotulia kuanzia maisha ya kawaida hadi ya kisiasa zake kutokana na wingi wa migogoro, mivutano na siasa dhaifu zilizokosa dira na tiba kwa miaka mingi sasa.
Migogoro hiyo imegeuka kuwa katili huku majeshi ya Serikali yakipambana na wanamgambo wa Boko Haram kaskazini mwa nchi na waasi watakao kujitenga wa eneo lizungumzalo Kiingereza (Anglophone) wakisumbua kaskazini na kusini magharibi mwa nchi.
Asilimia 20 ya wakazi milioni 24.6 wa taifa hilo wanazungumza Kiingereza na walio wengi Kifaransa.
Lakini utawala wa wanasiasa wazungumzao Kifaransa (Francophone) pasipo usawa ni chanzo cha mgogoro wa muda mrefu nchini humo.
Hilo linawakasirisha wazungumzao Kiingereza walio wachache waishio magharibi mwa nchi wanaolalamika kutengwa, kukandamizwa na kukosa uwakilishi wa kutosha na mfaidiko sawa wa ulaji wa keki ya taifa hilo.
Uwakilishi wa wanasiasa wazungumzao Kiingereza katika ngazi mbalimbali za kijamii umeanguka mno tangu Shirikisho la Jamhuri ya Cameroon lilipokuwa Jamhuri ya Muungano wa Cameroon mwaka 1972.
Ikumbukwe kabla ya 1961, eneo la kusini mwa Cameroon lilikuwa likitawaliwa na Uingereza kutokea Nigeria. Kisha likaunganishwa kujiunga na Jamhuri ya Cameroon.
Kutokana na kuwa na pande mbili sasa Francophone na Anglophones ikakubaliwa kuwepo serikali ya kugawana madaraka. Lakini makubaliano hayakuheshimiwa, Wazungumzao Kifaransa wakatumia wingi wao kukandamiza Anglophone, ambao uwakilishi ukazidi kupungua miaka hadi miaka,
Hali hiyo, ndiyo chanzo cha miito ya kutaka eneo hilo lizungumzao Kiingereza, kujitenga kutoka Cameroon huku likishuhudia migomo na maandamano ya mara kwa mara dhidi ya serikali.
Matumizi ya nguvu ya jeshi katika mgogoro huo na ule dhidi ya BokoHaramu ukashuhudia mamia wakiuawa na wengine 180,000 kukimbia makazi.
Wanaharakati wa Anglophone wanaotaka kuundwa kwa Jamhuri ya Ambazonia, wameonya kwamba hawataruhusu uchaguzi wowote utakaoendeshwa na utawala wa Yaoundé kufanyika katika ‘nchi yao.’
Lakini chama tawala Cameroon People’s Democratic Movement (CPDM kimeapa kwamba lazima uchaguzi ufanyike eneo hilo na kwamba Wacameroon wana haki ya kwenda kupiga kura au la.
Ushahidi wa kutisha wa mauaji yanayoendeshwa na majeshi ya usalama, ambayo yamejitokeza wiki za hivi karibuni yameashiria ukubwa wa matatizo yanayoikabili nchi.
Lakini Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 7, ambao ungepaswa kuleta suluhu ya matatizo hayo, unatarajia badala yake kuyaongeza.
Paul Biya, ambaye ameitumkia Cameroon kama rais kwa miaka 36, akiwa na umri wa miaka 85, kwa mastaajabu ndiye anayepewa nafasi kubwa ya kushinda muhula mwingine madarakani.
Lakini je, Wacameroon, ambao zaidi ya asilimia 60 ni vijana wenye umri chini ya miaka 35, wanaamini nchi yao iko katika mwelekeo sahihi?
Licha ya yote kuna viashiria fulani vinavyoibeba Cameroon. Ukuaji wa uchumi kwa ujumla unatia moyo licha ya kupunguza kasi yake katika miaka ya karibuni, na ukosefu wa ajira umeelezwa kuwa chini, hasa unapoulinganisha na mataifa jirani.
Lakini pia bado wananchi wengi wanaishi katika umasikini na nchi hii ni miongoni mwa mataifa 25 yanayoongoza katika orodha ya mataifa yanayonuka rushwa duniani kwa mujibu wa taasisi ya Transparency International.
Tofauti na viongozi wengine walio madarakani kwa miaka mingi, Biya si sehemu ya maisha ya kila siku ya Wacameroon wengi.
Akikosolewa kama rais kivuli kwa sababu ya safari zake ndefu na za mara kwa mara nje ya nchi, Biya huendesha shughuli za serikali kwa rimoti akiwa hotelini nje ya nchi kwa muda mwingi.
Baraza lake la mawaziri hukutana kwa nadra mno kama ilivyotokea mapema mwaka huu ikiwa ni mara ya kwanza kipindi cha miaka miwili.
Na maelezo yake ya kwanini anataka kuongoza kwa muhula mwingine wa saba madarakani ni kwamba eti watu wengi bado wanampenda na wamemshawishi kwa kumlilia na kumpigia magoti aendelee kubaki madarakani.
Hata hivyo, inahesabiwa kuwa mwiko kuzungumzia uking’ang’anizi wake madarakani.
April 2016, baadhi ya wafuasi wa upinzanin akiwamo mgombea urais wa mwaka 2011, Edith Kah Walla walikamatwa na kushikiliwa katika mji mkuu wa Yaoundé baada ya kuandamana kumpinga Biya na dhidi ya ukandamizaji wa sauti zinazopinga jaribio lake la kutaka kuwa ‘rais wa maisha.’
Hata hivyo, njia mpya kushughulikia tatizo hilo ya kumng’oa kihalali haionekani kuwa njiani bado.
Bado upinzani wa nchi hii licha ya kutamani kumng’oa Biya, umeparanganyika na mara nyingi hauna nguvu.
Wagombea 28 wamejitokeza kugombea urais, upinzani ukishindwa kukubaliana mgombea mmoja huku wengine 20 wakijitokeza kuwania kiti hicho cha enzi lakini wakimuunga mkono Biya. Ajabu sana!
Kila mfumo wa uwakilishi kidemokrasia na ufanisi hasa ujenzi wa ushirika imara wa upinzani, ambao ungepaswa kuwa suluhu hauna matumaini kabisa.
Pengine haishangazi, baadhi wameamua kuchukua uamuzi wa kutaka kujitenga. Cameroon inaonekana kukabiliana na si tu na kukosekana kwa uongozi fanisi bali pia uwapo wa siasa zilizoshindwa.
Rais Biya ni mtawala anayeshika nafasi ya pili kwa kutawala muda mrefu barani Afrika. Amepitwa na mwenzake wa Guinea ya Ikweta Teodoro Obiang’ Nguema Mbasogo tu kwa miaka mitatu. Biya aliingia kwa mara ya kwanza Ikulu Novemba 6, 1982, wakati taifa hilo likiwa chini ya mfumo wa chama kimoja.
Hata hivyo, licha ya taifa hilo kuwa katika zama za mfumo wa vyama vingi, Biya amefanikiwa kusalia mamlakani kwa miaka hii yote kwa mbinu zikiwamo ubabe, ulaghai na rushwa.
Mwaka 2011, baada ya Katiba ya taifa hilo kufanyiwa mabadiliko yenye utata ya kumruhusu kuwania kiti cha urais tena, alifaulu kushinda tena uchaguzi mkuu kwa asilimia 78 ya kura zote zilizopigwa na kusalia mamlakani kwa miaka mingine saba.
Ushindi huo mkubwa, uliwafanya wakosoaji wake wengi kuhoji na kushuku uhalali wa uchaguzi huo kiasi cha jina la mtaalamu wa wizi wa kura kumkaa vilivyo.
Akifahamika kama Simba Mtu’, jina la utani alilipata baada ya kudumu katika siasa za juu kwa muda mrefu, likitoka katika timu ya taifa ya mpira wa miguu, maarufu kama ‘Simba Wasioshindika,’ wakati ilipoingia robo fainali ya Kombe la Dunia mwaka 1990, kiongozi huyo lakini pia amekuwa akitumia mbinu za mnyama huyo tangu mwanzo.
Alizaliwa katika kijiji kilichopo kwenye msitu wa ikweta kusini mwa Cameroon, akaja someshwa na wamisionari wa Kikatoliki katika seminari ya karibu, akiwa na ndoto ya kuwa padri.
Lakini baadaye, akachagua kusomea sheria na sayansi ya siasa katika Chuo Kikuu cha Paris.
Alipohitimu akarudi nyumbani kufanya kazi katika utumishi wa umma.
Mtaalamu huyo mfupi akapanda ngazi akishika nyadhifa andamizi na kuondokea kuaminiwa na Ahmadou Ahidjo, ambaye alikuwa mkuu wa nchi tangu uhuru upatikane mwaka 1960.
Akawa waziri mkuu mwaminifu wa Ahidjo kwa miaka saba, hadi mwaka 1982 – wakati kwa mshangao wa wengi Ahidjo alipotangaza kujiuzulu urais na kumkabidhi madaraka Biya.
Ahidjo alishikilia uenyekiti wa chama tawala akidhani kuwa ulikuwa na nguvu zaidi kuliko nafasi ya urais.
Lakini Biya, alikuwa mwepesi katika kuvizia na kushambulia, akawaondoa wafuasi wa Ahidjo na hivyo kumlazimisha baba huyo wa uhuru kukimbilia uhamishoni.
Baadaye akajikuta akinusurika kupinduliwa mara mbili, tukio la kwanza likiwa mwaka 1983 na lingine mwaka mmoja baadaye.
Ahidjo alinyooshewa kidole kama mhusika mkuu wa njama hizo na mahakama ya kijeshi ikamhukumu adhabu ya kifo akiwa hayupo.
Kiongozi huyo wa uhuru akafariki dunia, baadaye nchini Senegal, na mwanafunzi wake huyu wa zamani aliyemgeuka hakuwa tayari kuuruhusu mwili wa mwalimu wake huyo kuletwa nyumbani kwa mazishi.
Biya pia alionesha ubaya kwa kipindi cha miaka mingi kwa washirika wake walioonesha kukinyemelea kiti chake hicho.
Mmoja wa madaktari wake yuko jela kwa tuhuma za rushwa, waziri wa zamani wa mambo ya ndani ndiyo ameanza hivi karibuni kutumikia kifungo cha miaka 25 jela kwa tuhuma kama hizo; waziri mkuu wa zamani anakabiliwa na kesi huku wengine wawili wakiwa wamekimbilia uhamishoni.
Hata hivyo, amekuwa akikwepa kujenga urafiki nao, akijiweka mbali na baraza la mawaziri – baadhi ya mawaziri wanateuliwa na kutimuliwa bila hata kuonana na rais kipindi chote wakiwa nyadhifani.
Katika jukwaa la kimataifa, pia ameonesha nguvu zake halisi – akimlazimisha jirani mwenye nguvu zaidi wa Cameroon, Nigeria kukabidhi Peninsula yenye utajiri ya Bakassi.
Awali nchi hizo mbili zilikuwa zimepambana mara kadhaa kugombea eneo hilo tajiri kwa mafuta na Biya aliamua kwenda katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki kuamua kesi hiyo.
Aidha Biya alidai kuwa anataka kukumbukwa kwa kuleta demokrasia nchini Cameroon.
Ni baada ya kusalimu amri kwa shinikizo la kuhitimisha mfumo wa chama kimoja na mwaka 1992 alishinda uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi nchini humo kwa asilimia 40 tu ya kura huku kukiwa na tuhuma za wizi wa kura.
Mpinzani wake mkuu, John Fru Ndi anaaminika kuwa alishinda uchaguzi huo, lakini Jaji wa Mahakama Kuu alimtangaza Biya mshindi.
Tangu, hapo rais akaja na mbinu zilizomshuhudia akishinda uchaguzi mmoja baada ya mwingi na hajawahi kupata chini ya asilimia 75 ya kura.
Wakosoaji wake wanasema rais na washirika wake wamehakikisha Wacameroon hawana chaguo lingine zaidi yake, huku chama chake kikihakikisha kinashinda kila chaguzi kwa kutumia mbinu zote.
Ni hilo lililomfanya pia abatizwe kuwa mtaalamu wa wizi wa kura.Na rushwa ni suala lililotawala uongozi wa Biya kipindi chote akiwa madarakani.
Licha ya kuanzisha tume ya kuzuia rushwa, bado saratani hiyo adui wa haki imejikita mizizi katika kada zote za jamii na kukwamisha maendeleo ya nchi, na kuifanya Cameroon ishinde taji kama nchi inayonuka rushwa kuliko zote duniani mara mbili katika miaka ya 1990.
↧
DC AAGIZA VICHANGA KUCHUNGUZWA UKEKETAJI
NA RAPHAEL OKELLO-BUNDA
MKUU wa Wilaya (DC) ya Bunda, Lydia Bupilipili, ameagiza wahudumu wa afya na madaktari wilayani hapa kuhakikisha wanawafanyia uchunguzi watoto wote wachanga wanaofika kwenye kliniki, vituo vya afya na zahanati kama wamefanyiwa ukeketaji.
Hatua hiyo inatokana na madai ya kuwapo kwa vitendo vya ukeketaji wilayani hapa, ambavyo hufanyika kwa siri hasa kwa watoto wachanga mara tu wanapozaliwa.
“Ukeketaji ni ukatili, ni jambo lisiloweza kuvumilika, kwahiyo natoa agizo kwa madaktari na wauguzi fanyeni uchunguzi na kwa wale wote watakaobainika kuwafanyia ukeketaji watoto wachanga sheria
ichukue mkondo wake,” alisema Bupilipili.
Awali akiwasilisha taarifa ya hali ya unyanyasaji na ukatili wa kijinsia wilayani Bunda, Mkurugenzi wa Shirika la Zinduka, Maximilian Madoro, alisema ukeketaji unafanyika kwa usiri mkubwa tofauti ilivyo katika wilaya za Tarime na Serengeti.
“Ukeketaji katika Wilaya ya Bunda hauambatani na sheria na matangazo kama ilivyo katika wilaya nyingine na ili kubaini
hali hiyo uchunguzi wa kina unatakiwa kufanyika kuhusu hali ya ukeketaji wa watoto wa kike,” alisema.
↧
WANAOPOTEZA PASIPOTI KUTOZWA SH 500,000
Na SHEILA KATIKULA-MWANZA
IDARA ya Uhamiaji imewaonya wanaopoteza hati za kusafiria watalazimika kulipia upya kati ya Sh 500,000 na 750,000 badala ya Sh 130,000 ya awali.
Hayo yalisemwa juzi na Naibu Kamishna wa Uhamiaji Mkoa wa Mwanza, Paul Eranga, wakati wa uzinduzi wa utoaji hati mpya za kusafiria za kisasa za kielektroniki (pasipoti).
Alisema kumekuwa na wimbi kubwa la watu kusingizia kupotea kwa pasipoti zao, hivyo uamuzi wa Serikali kwa sasa ni kuwatoza malipo ya ziada kama adhabu kwa wale ambao watapoteza.
Kamishna huyo pia alisema baadhi ya raia wamekuwa wakisingizia kupoteza pasipoti zao kwa lengo la kupata mpya pale wanapokwenda nchi za nje na kufanya makosa.
“Wakienda nje na kufanya makosa, pasipoti zao huwekwa kwenye kundi la watenda makosa, hivyo husingizia zimepotea ili wapewe zingine mpya kuondoa kumbukumbu hiyo.
“Kwa sasa ukipoteza pasipoti yako kwa mara ya kwanza utalipa Sh 500,000 kuipata mpya, hii ikiwa na malipo ya adhabu kwa kuwa mzembe kiasi cha kupoteza, lakini ukipoteza tena kwa mara ya pili, basi utalazimika kupata nyingine kwa gharama ya Sh 750,000,” alisema.
Alisema uamuzi huo umefikiwa kwa kuwa watu wengi wamekuwa wakiichukulia pasipoti kama jambo la kuchezea, hivyo lengo la Serikali kuwatoza gharama kubwa ni kutoa adhabu ambayo itawafanya kuwa makini na kuitunza kama nyaraka muhimu.
Eranga alisema tangu Januari 31, mwaka huu utoaji pasipoti mpya ulipozinduliwa, tayari wamepokea maombi 30,941 na kuyafanyia kazi, hivyo aliwataka wananchi kuchangamkia fursa kwa kuwa mfumo wa sasa ni rahisi, kwamba mtu anaweza kupata pasipoti ndani ya saa moja au siku moja.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela akizindua huduma hiyo, alitoa wito kwa wananchi kutoa taarifa mapema pale wanapobaini au kuwa na shaka na mtu asiye raia ili hatua za kisheria zifuatwe.
Aidha aliwaagiza maofisa uhamiaji kufanya kazi zao kwa uadilifu na kwa kuzingatia sheria, taratibu na miongozo iliyowekwa na Serikali ikiwa ni pamoja na kutoa huduma stahiki.
↧
Alex Song: Former Cameroon and Arsenal midfielder signs for Sion
Former Cameroon and Arsenal midfielder Alex Song signs a two-year deal with Swiss top-flight club Sion.
↧
↧
London terror suspect identified as Briton of Sudanese origin
British media have named the man behind Tuesday's suspected terror attack outside the Houses of Parliament. Police have said they are still investigating the suspect's motives.
↧
Senator's 'White Australia' speech sparks uproar
Senator Fraser Anning delivered a racist speech to parliament that has drawn condemnation. The freshman senator defended his use of the term "final solution" to hold a vote on immigration.
↧
Serikali ya Misri yawatoa kifungoni mashabiki
SERIKLI ya Misri kupitia Waziri wa Michezo, Ashraf Sobhy ametangaza rasmi kuwaruhusu mashabiki wa mpira wa miguu kuingia uwanjani katika michezo ya Ligi Kuu nchini humo toka walipopigwa marufuku mwaka 2012. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea). Mashabiki hao walifungiwa kuingia uwanjani toka 1 Febuari, 2012 baada ya vurugu kubwa kuibuka katika mchezo uliowakutanisha Al Masry ...
↧