A pair of mass shootings in Texas and Ohio over the Saturday and Sunday have dragged two of the most divisive issues in American politics -- the rise of violent white supremacism and gun control -- to the forefront of public conversation as politicians across the ideological spectrum are preparing for what is expected to be an extremely contentious 2020 election campaign.The two shootings, which left 29 people dead and at least 53 more wounded, combine to create a clear political crisis for the Trump administration and its allies in Congress.The first shooting, in El Paso, Texas, occurred early Saturday and was carried out by a 21-year-old white man who is believed to have published an explicitly racist manifesto that echoed U.S. President Donald Trump’s frequent charge that Hispanic immigrants from Mexico and Central America constitute an “invasion” of the United States. After he surrendered, he told police that he had set out to kill as many “Mexicans” as he could. He murdered 20 people and wounded another 27.The second, in Dayton, Ohio, was committed after 1 a.m. Sunday by a 24-year-old white man toting a legally-purchased military-style semi-automatic rifle equipped with two 100-round drum magazines that helped him kill or injure three dozen people in less than 30 seconds. President Trump and Republican lawmakers have been adamantly resistant to the kind of regulations promoted by Democrats that would make it impossible for a private citizen to amass such firepower.The murders in the Texas border city of El Paso come at a time when violence related to white supremacist ideologies is demonstrably on the rise. In July, Federal Bureau of Investigation Director Christopher Wray told Congress that the “majority of the domestic terrorism cases we’ve investigated are motivated by some version of what you might call white supremacist violence.”A man leaves flowers near the scene of a mass shooting at a shopping complex, Aug. 4, 2019, in El Paso, Texas.A killer's manifestoIn 2018, domestic terrorists killed at least 50 people in the U.S., according to the Anti-Defamation League Center on Extremism, which tracks such murders. Every one of the killers had an identifiable connection to a right-wing political movement, the center said.In what is believed to be his manifesto, the El Paso killer made it clear that his antipathy toward Hispanics pre-dated Trump’s rise to power in the 2016 election, but the similarity of some of his language to the president’s rhetoric in his campaign rallies was unmistakable.Like Trump, the killer described immigrants as “invaders.” At recent political events, Trump has called for minority members of Congress to “go back” to the places they came from. In his manifesto, the killer said that “patriotic Americans” should give immigrants the “right incentive” to return to their home countries.Most notably, perhaps, is that while railing against illegal immigrants during a re-election rally in May, the president asked the crowd “How do you stop these people?” When one supporter shouted “Shoot them!” Trump laughed as the crowd roared its approval.On Sunday, acting White House chief of staff Mick Mulvaney made multiple TV appearances to defend the president from a chorus of accusations -- most notably from Democratic presidential candidates -- that Trump’s rhetoric fans the flames of violent white supremacism.“This was a sick person. The person in Dayton was a sick person,” Mulvaney said in an appearance on ABC News. “No politician is to blame for that. The person who was responsible here are the people who pulled the trigger. We need to figure out how to kind of create less of those kinds of people as a society and not trying to figure out who gets blamed going into the next election.”Mulvaney was then pressed on Trump’s seeming reluctance to identify white supremacism as a significant concern. After a gunman spouting white supremacist rhetoric murdered dozens of Muslims in New Zealand earlier this year, Trump was asked if he views the ideology as a global threat. He responded: “I don’t really. I think it’s a small group of people that have very, very serious problems.”“I don't think it's at all fair to sit here and say that he doesn't think that white nationalism is bad for the nation,” Mulvaney said. “These are sick people. You cannot be a white supremacist and be normal in the head.”Mick Mulvaney, as Acting White House Chief of StaffBut Democrats, particularly presidential candidates, were having none of it.Speaking on Meet the Press on Sunday morning, New Jersey Sen. Corey Booker described Trump as “particularly responsible" for the uptick in violence by white supremacists. “In my faith, you have this idea that you reap what you sow, and he is sowing seeds of hatred in this country, this harvest of hate violence that we are seeing right now lies at his feet,” Booker said.“There is a complicity in the president's hatred that undermines the goodness and decency of Americans,” Booker added.Julián Castro, the former mayor of San Antonio and the Secretary of Housing and Urban Development in the Obama administration, said on Sunday that Trump was not directly responsible for the shooting in El Paso. However, he said that the president’s rhetoric toward immigrants had contributed to a surge in white nationalism in the U.S.Beto O’Rourke, the former Texas congressman who calls El Paso home, may have been the most forceful in tying Trump to the killings there. Appearing on CNN, he responded in the affirmative when asked if he believes the president is a white supremacist. “The things that he has said both as a candidate and then as the president of the United States? This cannot be open for debate,” he said.“We have a problem with white nationalist terrorism in the United States of America today," O'Rourke added. “These are white men motivated by the kind of fear that this president traffics in.”"Hate has no place in this country"For his part, Trump himself made little in the way of public statements Sunday. Returning to the White House from one of his golf resorts in the afternoon, the president made brief comments to the media. “Hate has no place in our country and we’re going to take care of it,” he said.As the day went on, and more information came to light about the killings in Dayton, Democrats – already calling for Republicans to relent on passage of gun control measures in Congress -- only got louder in their calls for limiting access to firearms.Their complaints were directed, sometimes explicitly and sometimes indirectly, at Republican lawmakers who have actively resisted efforts to tighten access to firearms. Most recently, Senate Majority Leader Mitch McConnell has blocked votes on a popular bill to expand mandatory background checks on people looking to purchase firearms and a more controversial proposal that would ban the sorts of weapons used in the El Paso and Dayton attacks.On Twitter, Massachusetts Sen. Elizabeth Warren urged Senate Majority Leader Mitch McConnell to "bring the Senate back from recess to vote on legislation to address the gun violence epidemic.”We must treat this like the public health crisis that it is. @SenMajLdr: Bring the Senate back from recess to vote on legislation to address the gun violence epidemic.— Elizabeth Warren (@ewarren) August 4, 2019South Bend, Indiana Mayor Pete Buttigieg tied the two events together, saying, “America is under attack from homegrown white nationalist terrorism...And we have to talk and act about two things in this country. First of all, we are the only country in the world with more guns than we have people. We can respect the Second Amendment and not allow it to be a death sentence for thousands of Americans, and two, white nationalism is evil."
↧
US Mass Shootings Stoke Issues of White Supremacism and Gun Control
↧
Zoezi La Kupima Utayari Wa Kukabili Ebola La Acha Alama Mkoani Kagera
Na. OWM, KAGERASerikali kupitia uratibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Menejimenti ya Maafa kwa kushirikiana na Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, pamoja na wadau wa maendeleo, imefanikiwa kufanya zoezi la kupima utayari wa kukabili ugonjwa wa Ebola katika mkoa wa Kagera katika wilaya tatu za mkoa huo kwa kuhusisha watoa huduma za Afya katika wilaya hizo za Bukoba, Misenyi na Ngara.Zoezi hilo limefanikiwa kuwaimarisha watumishi hao katika maeneo maalum ikiwemo ya uratibu, utambuzi na ufuatiliaji wa wagonjwa iwapo wakipatina, matibabu ya wagonjwa, uchukuaji na usafirishaji wa sampuli na kuthibitisha maabukizi pamoja kuimarisha mifumo ya utambuzi wa masuala ya Afya kwa kila abiria wanaopita kwenye mipaka ya mkoa wa Kagera.Akiongea kuhusu kuhitimishwa kwa zoezi hilo jana tarehe 3 Agosti, 2019, mkoani Kagera, Mkurugenzi Msaidizi (Utafiti na Mipango), Idara ya Menejimenti ya Maafa, ofisi ya Waziri Mkuu, Bashiru Taratibu, ameeleza kuwa watumishi wa sekta ya Afya katika maeneo yote ambayo zoezi hilo limefanyika wameweza kuimarishwa katika suala la uratibu hususani katika kuhakikisha kuwa rasilimali zote zinazohitajika pindi ikigundulika kuwepo kwa mgonjwa wa Ebola zinapatikana kwa wakati na kwa kutosheleza mahitaji pamoja na kutumika kwa usahihi.Aidha, Mratibu wa zoezi hilo toka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, ambaye pia ni Mtaalamu wa Afya ya Jamii, Dharura na Maafa, Dkt. Faraja Msemwa amefafanua kuwa timu ya wataalamu wa sekta za Afya na Uratibu wa Shughuli za serikali, kutoka Wizarani, Idara na Mashirika ya Kimataifa, wamefanikiwa kuendesha zoezi hilo kwa watoa huduma wa Afya kwa wilaya tatu za mkoa huo hususan zilizopo mipakani.“Zoezi letu tumefanikiwa kulihitimisha mkoani hapa tayari kwa kufanya zoezi la kupima utayari wa kukabili ugonjwa wa Ebola kwa watoa huduma wa Afya kwa vituo vya Afya vya Nshambya, Kabyaile, Kabanga, Bunazi pamoja na Hospitali ya Rufaa ya mkoa ya Bukoba.Tunaamini kufanikiwa kufanya zoezi hili limeboresha utendeji wa watoa huduma hao katika kukabili ugonjwa wa Ebloa” alisema Dkt. MsemwaKwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa huo, Dkt. Marco Mbata amefafanua kuwa kufanyika kwa zoezi hilo mkoani humo kumewawezesha kujua maeneo gani ya kuboresha wakati wa ugonjwa wa Ebola na watumishi wameelewa kwa vitendo wapo tayari kukabili ugonjwa huo.“Tunashukuru vifaa tunavyo vya kutumia wakati wa kujikinga iwapo atatokea mgonjwa wa Ebola, hivyo kupitia zoezi hili tumeongeza uelewa wa kujikinga wenyewe, kuwakiknga watu walio karibu na mgonjwa pamoja na jamii nzima. Tumeweza kujifunza jinsi ya kumpokea mgonjwa, kuchukua vipimo hakika zoezi hili limetujenga ” alisisitiza Mbata.Naye Mratibu wa Vituo vya Mipakani, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Remedius Kakuru amebainisha kuwa kupitia zoezi hilo limeimarisha utendaji wa maafisa Afya wa mipakani kwa kuzingatia kuwa tayari serikali imenunua vifaa vya kisasa muhimu vinavyo hitajika kwa ajili ya utambuzi wa abiria mwenye maambukizi ya ugonjwa wa Ebola ikiwemo Vipima joto la mwili “themo scanners”.Vifaa hivyo vyenye uwezo wa kupima joto la mwili la abiria wanao pita katika mipaka ya Tanzania vina uwezo wa kupima joto la mwili kwa kuwa ndiyo kiashiria kikuu kimojawapo kwa mgonjwa mwenye maabukizi ya Ebola .Kwa upande wake Afisa anayeshughulika na Magonjwa ya Mlipuko kutoka Shirika la Afya Duniani, hapa nchini, Anthony Kazoka alieleza kuwa Shirika la Afya Duniani linaendelea kushirikiana na serikalai ya Tanzania katika kulinda Afya za watu wake kwa kutoa utaalamu katika zoezi hilo kwa kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo zimo hatarini kupata mlipuko wa ugonjwa wa Ebola. Hivyo kwa kufanyika zoezi hilo kwa mafanikio kutasaidia Tanzania kuwa salama na kuwa chanzo cha kuiweka Dunia salama kwa kutambua maabukizi ya ugonjwa huo mapema iwapo yatatokea.Kufuatia nchi ya jirani (DRC) kuendelea kukabiliwa na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola tangu Agosti mwaka 2018. Tanzania imeendelea kuchukua tahadhari za ugonjwa huo kwa kupima utayari wa Watoa huduma za Afya kwa mikoa ya mipakani ukiwemo mkoa wa Kagera. Mkoa huo ambao unapakana na nchi ya Uganda ambayo inapakana na DRC lakini pia imekuwa na wagonjwa kadhaa wa Ebola.Zoezi hilo linaratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa ushirikiano na wadau wa maendeleo ambao ni WHO, FAO, USAID, HRH2030, na USAID Global Health Supply Chain Programu. Zoezi hilo limefanyika kwa muda wa wiki moja ambapo limekamilika tarehe 3 Agosti mwaka 2019, kwa kufanyika katika vituo vya kutolea huduma za afya na maeneo ya mipaka ya mkoani wa Kagera.MWISHO.
↧
↧
Mwalimu adaiwa ampachika ujauzito mwanafunzi wake
MOHAMED HAMAD-KITETO
JESHI la Polisi Wilayani Kiteto Mkoani Manyara, linamshikilia
mwalimu, Daniel Saulo wa Shule ya Msingi Matui kwa tuhuma za kumpachika
ujauzito mwanafunzi wake wa darasa la saba.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, RPC Christopher Foime,
amethibitisha tukio hilo kwa kukamatwa mtuhumiwa huyo na yuko Kituo cha Polisi
Matui kwa ajili ya upelelezi na uchunguzi zaidi.
“Kwa sasa mtuhumiwa tunamshikilia Kituo kidogo caha Polisi Matui,
anaendelea na mahojiano, atafikishwa mahakamani wakati wote taratibu
zitakapokamilika ili sheria ifuate mkondo wake,” alisema Kamanda Foime.
Akizungumzia tukio hilo Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Victoria Mushi,
alikiri kukamatwa mwalimu huyo akisema tukio hilo ni la tatu kujitokeza shuleni
hapo na kwamba hawezi kusema lolote kwa
sasa.
“Nilikuwa Kanisani sikupokea mapema simu yako, kuhusu suala hili la
mwalimu yupo Polisi kwa sasa siwezi kuzungumzia lolote, ingawa matukio haya
yamekuwa yakijirudia ni tukio la tatu, kwahiyo bado siwezi kusema lolote kwa
sasa ndugu yangu,” alisema Mwalimu Mushi alipokuwa anazungumza kwa njia ya
simu.
Akizungumza na MTANZANIA baba mzazi wa mtoto huyo, Isaka Maro
alielekeza masikitiko yake kwa Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Victoria Mushi kwa
kuficha tukio hilo ingawa alilifahamu toka mwanzo wiki wiki mbili zilizopita
baada ya shule kuwapima wanafunzi hao.
“Taarifa za kuwa mwanangu ana ujauzito wa miezi miwili nilizifahamu
toka kwa watu wiki mbili zilizopita ..nilipoenda shuleni kuuliza mwalimu Mkuu
alinificha ndipo nikaamua mwenyewe kumchukua mwanangu na kwenda kumpima kwenye
kituo cha Afya Engusero na kubaini haya,”alisema
Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Tumaini Magesa, alisema tatizo la watoto wa
kike kukatishwa masomo kwa kupachikwa mimba limekithiri, pamoja na kuwepo kwa
sheria Serikali inaendelea pia kuelimisha umma kuacha kuwapachika mimba
wanafunzi.
↧
Mzee wa miaka 95 aliyeombwa rushwa na polisi kumuona JPM
Abdallah Amiri-Igunga
MKAZI wa Kijiji cha
Isakamaliwa Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Ngaka Mataluma (95) na viongozi wa
CCM wa kata hiyo, wamepanga kuanza safari ya kwenda kuonana Rais Dk. John
Magufuli ili kushinikiza askari polisi sita wanaodaiwa kumuomba rushwa
wachukuliwa hatua za kisheria.
AskAri hao, ambao
wanadaiwa kuomba na kupokea rushwa ya Sh milioni 8 kutoka kwa Matalamu,
hawajachukuliwa hatua zozote na wakubwa zao, licha ya ushahidi kuwapo.
Akizungumza na MTANZANIA
nyumbani kwake mjini hapa juzi kwa niaba ya wenzake, Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji
cha Isakamaliwa Simon Makolo, alisema wamefikia uamuzi huo baada ya kuona
vyombo vya dola vimeshindwa kuchukua hatua stahiki.
Alisema wamepanga kuanza
safari ya kuonana na Rais Dk. Magufuli wakati wowote kuanzia sasa ili kufikisha
kilio chao.
“Wananchi wa Isakamaliwa, tumekuwa tukijiuliza
juu ya ukimya uliopo wa askari hawa na viongozi wawili wa Serikali ya Kijiji
cha Isakamaliwa, wanaotuhumiwa kuomba na kupokea rushwa ya shilingi milioni nane
kutoka kwa Mataluma kutofikishwa mahakamani.
“Hali imesababisha
Mataluma na viongozi wenzangu, tujipange kwa safari ya kwenda kuonana na rais,
tukiamini atatusaidia jambo hili ili haki itendeke,”alisema
Alisema amekuwa
akisumbuliwa na wananchi na Mataluma mwenyewe kutokana na kesi hiyo
kutofikishwa mahakamani tangu Juni 12, mwaka huu, lilipotokea tukio hilo.
Alisema yeye na viongozi
wengine, walitoa maelezo yao kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa
(TAKUKURU) na jeshi la polisi.
Alisema katika safari
hiyo, Mataluma atafuatana na Mwenyekiti
wa CCM tawi la Isakamaliwa, Nkwabi Galishi na mkazi wa kijiji hicho, Jilunga
Mwangali, viongozi wawili, mmoja wa serikali ya kijiji na mmoja wa chama ambaye
ni katibu wa tawi na mfanyabiashara
aliyenunua ng’ombe 11.
Alisema pamoja na hatua
hiyo, Mataluma amekuwa akisumbuliwa na mfanyabiashara Kashinje Mhela aliyenunua
ng’ombe wake 11 ambao alilazimishwa na polisi hao akitaka arudishwe fedha zake
Sh milioni 8.
“Ukimwangalia yule mzee
Mataluma amezeeka kweli kweli, sasa anasumbuliwa na huyu mfanyabiashara
arudishiwe fedha zake shilingi milioni 8 ambazo zinadaiwa kuchukuliwa na hawa
askari. Anaishi maisha ya hofu kila kukicha, jambo hili lazima lipate ufumbuzi,”alisema.
UHAMISHO
Pamoja na kilio cha
Mataluma, kuna taarifa za uhakika kutoka vyanzo vya jeshi la polisi Igunga,
kuwa askari wamehamishwa vituo vingine vya kazi katika wilaya za Sikonge, Uyui
na Nzega.
Inaelezwa Inspekta Frank
Matiku (36) ambaye aliongoza askari hao kwa kile kichodaiwa rushwa, amehamishiwa
Wilaya ya Sikonge kuwa Mkuu wa Upelelezi Msaidizi, PC Raphael Maloji (31) na Koplo
Paulo Bushishi (49), wanahamishiwa Wilaya ya Uyui, DC Lucas Nyoni (31), PC Lome
Laizer (39) na Koplo Charles Zacharia (45), wamehamishiwa Wilaya ya Nzega.
Mkuu wa Wilaya ya Igunga,
John Mwaipopo alipoulizwa juu uhamisho huo jana, alisema yeye hajapata taarifa
yoyote.
Kwa upande wake, Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Tabora, Barnabas Mwakalukwa alipoulizwa alisema hana taarifa hizo.
“Umezipata taarifa hizi wapi,
mimi ndio naingia Tabora, nitafuatilia,” alisema Mwakalukwa.
Hivi karibuni, Mkuu wa Takukuru
Mkoa wa Tabora, Chaulo Mussa alisema wanasubiri askari hao wafukuzwe kazi na mwajiri wao ili wawafikishe mahakamani.
Juni 12, mwaka huu katika Kijiji
cha Isakamaliwa, askari hao na Mwenyekiti wa Kitongoji cha Zahanati, Juma
Mwagala na Ofisa Mtendaji wa Kijiji chicho, Edward Kitenya walituhumiwa kuomba
na kupokea rushwa ya milioni 8 kutoka
kwa Mataluma, wakimtuhumu kujihusisha na vitendo vya upigaji ramli chonganishi,
kumiliki nyara za serikali, zikiwamo ngozi ya kenge na bunduki aina ya gobole.
↧
Dk. Bashiru apiga marufuku vikao vya fitina CCM
CLARA MATIMO Na YOHANA PAUL- MWANZA
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Bashiru Ally, amepiga
marufuku vikao vya fitina ambavyo vinalenga kujadili ajenda kabla ya wakati.
Alitoa onyo hilo jijini hapa mwishoni mwa wiki katika mkutano wa
kuimarisha demokrasia mashinani uliofanyika katika Uwanja wa CCM Kirumba.
Dk. Bashiru ambaye pia ni mlezi wa CCM Mkoa wa Mwanza, alisema vikao vinavyoruhusiwa ni vile
vinavyojadili utekelezaji wa ilani ya CCM, kero za wananchi na wanachama,
kutatua migogoro kwa mujibu wa taratibu na
kufanya uteuzi wa watu wenye sifa.
“Najua tunaelekea kwenye vikao vya uchaguzi ni marufuku kuendesha
vikao vya fitina vile vilivyozoeleka watu wanapanga na kujadili ajenda kabla ya
wakati na wanatoka wamedhamiria kuchinja mtu,
pia ikiwa ni kikao cha siri, siri hizo zisivuje, katika kipindi hiki
ndani ya CCM ni marufuku kulea na kufuga makundi ya vyeo.
“Kuna eneo nimesikia mtu mmoja amechinjwa baada ya kushinda kura za
maoni wakampeleka mtu wa pili kwa kisingizio kwamba alikuwa Chadema sasa nasema
hivi wote waliorudi CCM kwa kufuata utaratibu wa kikatiba tangu saa hiyohiyo
wana haki na wajibu sawa na wanachama wengine.
“Kama vitendo vya kuchinja mtu vinafanyika mikoa mingine Mkoa wa
Mwanza ambako mlezi ni mimi upokee pesa kwa njia yoyote halafu umwambie
nitakupigia debe kwenye vikao, upitishe mtu asiye na sifa kisa ulisoma naye au
mnajuana kwa namna yoyote ile hapa hakuna tena nafasi hiyo na ukibainika
utachukuliwa hatua za kinidhamu,” alisema.
Aidha Dk. Bashiru alisema wataendelea kuboresha elimu ya msingi na
sekondari kwa kuwajengea wanafunzi mbinu
za kujitegemea ikiwemo kukuza uwezo wa kufikiri, kuchambua
mambo mbalimbali , kujiamini, kubuni na kupenda taifa lao .
“Tunataka watoto wetu wawe wabunifu na waweza kujiamini wasisome tu
kwa ajiri ya kujibu na kufaulu mitihani na kujaza lundo la vyeti la hasha!
tunataka wawe kama viongozi wetu
waliotangulia akiwemo Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere ambaye tumampa sifa
nyingi kutokana na kupata elimu yenye utaifa ndani yake.
“Wako wasomi mnawajua wanamalundo na magunia ya vyeti wengine
wanaitwa maprofesa, wengine wasomi mawakili na wachumi lakini hawajiamini na
hawana utaifa, msomi aliyesoma na kusomeshwa katika nchi hii hawezi kunyanyua
kinywa chake kumtusi rais, usomi wa aina hiyo ni laana,” alisema na kuonya Dk.
Bashiru.
↧
↧
Simanzi mazishi mke aliyeuawa kuchomwa moto Simanzi yatawala mazishi mke aliyeuawa na mume
Andrew Msechu-DAR ES SALAAM
NI simanzi. Ndivyo unaweza kusema,baada ya
mamia ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, kukusanyika na kushiriki mazishi ya
Naomi Marijani, ambaye anadaiwa kuuawa na mume wake, Khamisi Luwongo, kisha
kuteketeza mwili wake kwa kuuchoma moto.
Inadaiwa Naomi, alitoweka katika mazingira
ya kutatanisha Mei, mwaka huu, ambapo picha na taarifa zilizodaiwa kuandaliwa
na mumewe Luwongo, zilisambazwa kwenye mitandao ya kijamii zikidai
atakayefanikisha kupatikana kwake, atapa zawadi ya Sh milioni moja.
Kutokana na taarifa hizo ambazo baadaye,
Kamanda Polisi Mkoa wa Kipolisi Temeke, Amon Kakwale, alisema Mei 19, mwaka huu, Luwongo alifika
katika Kituo cha Polisi Gezaulole, Kigamboni na kufungua jalada la taarifa kuwa
mkewe, Naomi ametoroka.
Alisema kama ilivyo taratibu za polisi,
walianza uchunguzi na Juni 12, Luwongo
alifika tena kituoni hapo na kueleza kuwa
mke wake, ametelekeza mtoto wao anayeitwa Grecious (7).
Jana ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu
Naomi, walikusanyika nyumbani kwa kaka yake Mbweni, Dar es Salaam na kufanya
ibada wa mazishi kama ishara ya kutimisha msiba wake.
Katika ibada hiyo, pia ilihudhuriwa na
majirani wa Naomi waliokuwa wakiishi naye Kigamboni pamoja na vikundi
mbalimbali vya kwaya.
Akizungumza wakati wa ibada hiyo ya
mazishi, Mchungaji wa Kanisa alilokuwa akisali marehemu Naomi la Sabato Gezaulole, Jackob Chimbwegu, alisema wakati wote wa uhai
wake marehemu alikuwa mshirika mzuri ambaye alisababisha kununuliwa kwa viti
vya kisasa plastiki.
“Tumeguswa sote, kwa kilio cha maumivu
mliyonayo ndugu, hakuna namna ya kuwatuliza. Zaidi ni kumwomba Mungu awatulize
mnaopita katika wakati huu mgumu,” alisema Mchungaji Chibwengu
Pamoja na hali hiyo, aliwataka
waombolezaji kujiweka tayari kuonana na Mungu kwa kuwa katika maisha ya
binadamu ni mafunzo tosha, kwani hakuna anayejua atakavyoondoka hapa duniani.
Naye Mchungaji Emmanuel Mhando wa Kanisa
la FPCT, alisema kuna maswali mengi watu wanaweza kujiuliza, kwa nini Naomi,
kwa nini kifo kiwe cha namna hii?
Alisema kwanini zinakuwa nyingi, lakini hakuna
haja ya kulalamika tena, hakuna haja ya kujiuliza, bali kuomba nguvu ya kusonga
mbele.
“Ni imani yangu baada ya ibada hii,
tusiendelee kulaumu, tuseme inatosha, inatosha, tumuombe Mungu atupe nguvu ya
kusonga mbele,” alisema Mchungaji Mhando
KAULI YA FAMILIA
Kwa upande wake,msemaji wa familia,
Wiseman Marijani alisema jambo lililowasibu ni zito na gumu wakati wote
walikuwa wamezongwa na hawakujua nini cha kufanya.
Alisema familia inapenda kumshukuru Mungu
kwa mambo makuu, tangu Naomi aliyedaiwa
kupotea Mei 15, mwaka huu, lakini wakaja kujua aliko siku 60 baadaye.
“Tulianza kukata tama, Mungu alitufungulia
fumbo na kujua aliko Naomi, baada ya mbingu kumlazimisha Meshack, mumewe
kueleza kinagaubaga kuhusu ukatili alioufanya, alisema.
Alisema anaushukuru uongozi wa Wizara ya
Mambo ya Ndani ya Nchi na Jeshi la Polisi, vyombo vya habari pamoja na wananchi
ambao walisaidia kupata taarifa za haki aliko Naomi.
Alisema taarifa zilizosaidia kujulikana
aliko Naomi zilipatina kutoka kwa msamaria ambaye aliwapa mbinu iliyosaidia
kutanzua fumbo hilo
Alisema kwa kuwa suala hilo liko
mahakamani, wanaiombea mahakama iweze kutoa haki stahiki.
Alisema baada ya ibada maalumu kufanyika
jana, familia itaendelea kusubiri mamlaka husika ili ziwarejeshee mabaki ya
mwili wa Naomi ili waweze kumpumzisha kwa amani.
TAARIFA ZA KUUAWA
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa
Kipolisi Temeke, Amon Kakwale alisema baada ya utata wa taarifa za tukio hilo,
polisi walianza utaratibu wa uchunguzi
ambapo Juni 12, Luwongo alifika tena kituo hicho cha polisi na kueleza
kuwa Naomi ametelekeza mtoto anayeitwa Grecious mwenye umri wa miaka saba.
Kamanda huyo alisema baada ya Jeshi la
Polisi kupokea taarifa hizo, kesi hizo zilianza kufanyiwa kazi.
Alisema wakati wanaendelea na uchunguzi
juu ya suala hilo, ndugu wa Naomi nao walifika katika kituo cha Polisi
Chang’ombe, wakieleza kuwa ndugu yao alikuwa amepotea na wana shaka na mumewe
kuhusu kutoweka kwake.
Alisema kutokana na maelezo hayo ya ndugu
wa Naomi, Jeshi la Polisi likamtia mbaroni Luwongo kwa ajili ya mahojiano.
Alisema Julai 15, akiwa mbele ya jeshi
hilo akaeleza taarifa alizokuwa ameeleza awali hazikuwa za kweli na akaanza
kueleza ukweli wa namna mkasa mzima ulivyokuwa.
Julao 30, mwaka huu, mume aliyekuwa
akishikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kumuua mkewe, kisha kumchoma kwa
mkaa magunia mawili ya mkaa na kumzika shambani kwake, Khamisi Luwongo
(Meshack), alifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kusomewa mashtaka
yanayomkabili.
Luwongo, alifikishwa mahakamani hapo na
kuwekwa mahabusu ya mahakama hiyo akisubiri kupangiwa Hakimu.
Hata hivyo, jalada la kesi ya mauaji ya kukusudia limepangwa kusikilizwa
mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustine Mmbando.
Mshtakiwa anatuhumiwa kumuua mkewe Naomi (36), Mei mwaka
huu katika maeneo ya Kigamboni,Dar es Salaam.
↧
Barcelona yaizima Arsenal
Bao lililofungwa na Luis Suarez dakika ya 90 limeinyoa Arsenal katika mchezo wao wa kirafiki uliochezwa jana kwenye Uwanja wa Nou Camp.
↧
Dili la Dybala Man United utata mtupu
Ndoto ya Manchester United kumsajili Paulo Dybala imeanza kufutika baada ya mshambuliaji huyo kutaka dau kubwa la mshahara.
↧
Carrie Lam warns Hong Kong in a 'very dangerous situation'
Hong Kong leader Carrie Lam has made her first media appearance in days amid mass anti-government protests. Lam condemned the violence and said that protesters should "say no to chaos".
↧
↧
Tanzania Yalaani Mauaji Ya Watu Wasio Na Hatia Marekani
↧
Jaji Mstaafu Wa Mahakama Kuu Ya Tanzania, Mhe. Jaji Rugazia Afariki Dunia
Jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Projestus Aloyce Rugazia (pichani) amefariki dunia. Mhe. Jaji Rugazia amefariki dunia alfajiri ya kuamkia Agosti 04, 2019 akiwa anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa-Muhimbili jijini Dar es Salaam. Msiba upo nyumbani kwake Kinondoni- Dar es Salaam, ratiba ya taratibu za kuaga na mazishi itajulikana mapema Agosti 05, 2019. Marehemu Jaji Rugazia alizaliwa Agosti 28, 1954 mkoani Kagera, alianza kazi rasmi Januari 01, 1983 kama Hakimu Mkazi. Marehemu aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu Machi 28, 2003. Aidha; Marehemu Jaji Rugazia alistaafu rasmi Agosti 28, 2016 akitokea Mahakama Kuu-Divisheni ya Ardhi. Mahakama ya Tanzania imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo chake. BWANA AMETOA, BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE IMETOLEWA NA : KITENGO CHA HABARI, ELIMU NA MAWASILIANO, MAHAKAMA YA TANZANIA.
↧
Katibu Mkuu Wizara Ya Fedha Awataka Watafiti Na Wadadisi Kuzingatia Viwango Ukusanyaji Wa Takwimu
Na Mwandishi Wetu, MAELEZOKATIBU Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Doto James amewataka wadadisi na wasimamizi wa utafiti wa sekta isiyo rasmi nchini kuzingatia viwango vya ubora katika ukusanyaji wa taarifa ili kuiwezesha Serikali kupata takwimu sahihi zenye kubaini mahitaji na changamoto za sekta hiyo nchini.Akizungumza katika Ufunguzi wa Mafunzo ya Wadadisi na Wasimamizi wa Utafiti wa Sekta isiyo rasmi Nchini jana Jumapili (Agosti 4, 2019) Jijini Dar es Salaam, Bw. James alisema matokeo ya utafiti huo yataisaidia Serikali kufahamu mchango halisi wa sekta isiyo rasmi katika Pato la taifa ikijumuisha ulipaji kodi.Aliongeza kuwa ni ukweli ulio dhahiri kuwa sekta isiyo rasmi imekuwa nguzo muhimu katika pato la taifa kwani kulingana na utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi uliofanyika mwaka 2014 ilibainika kuwa, asilimia 21.7 ya watu waliokuwa na ajira walikuwa katika sekta isiyo rasmi, na hivyo kuleta kiashiria kuwa sekta hiyo ina mchango muhimu katika pato la taifa.Bw.James alisema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imejiwekea malengo mbalimbali katika kuinua uchumi wa wananchi wake ikiwemo kubaini changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta isiyo rasmi ikiwemo hali ya upatikanaji wa masoko, fursa za mikopo, ujuzi unaohitajika pamoja na matumizi ya teknolojia kwa nia ya kuongeza tija kwenye uzalishaji.“Sina shaka na ubora wa takwimu zitakazokusanywa kwa kuwa mnaendelea kufanya kazi hii kwa karibu sana na Shirika la Kazi Duniani (ILO) na Benki ya Dunia (WB), tumieni uzoefu wenu ili na sisi Watanzania tunufaike kuifahamu zaidi sekta hii katika kukuza uchumi wa Tanzania” alisema Bw. James.Kwa mujibu wa Bw. James alisema utafiti wa kwanza wa kitaifa katika sekta isiyo rasmi ilifanyika nchini mwaka 1991 na kufuatiwa na utafiti kama huo katika Mkoa wa Dar es Salaam mwaka 1995, hivyo ni kipindi kirefu kimepita na kufanya kuwepo na mahitaji makubwa ya takwimu zinazoakisi hali halisi ya sasa ya sekta hiyo nchini.Kwa upande wake, Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Dkt. Albina Chuwa alisema hatua ya Serikali ya Awamu ya Tano kufanya utafiti huo ni uthubutu mkubwa kwa Tanzania kwa kuwa ni nchi chache za Bara la Afrika zimeweza kufanya utafiti huo kwa ajili ya kupima sekta yenyewe na upatikanaji wa rasilimali fedha sambamba na kubaini fursa za ajira kwa wananchi wengi wakiwemo wananchi maskini.“Kama mnayofahamu Serikali kwa sasa inatekeleza Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa wa mwaka 2016/17 hadi 2020/21 ambao unahitaji takwimu katika ngazi za chini za utekezaji, ili kuongeza wigo wa hifadhi ya jamii kwa lengo la kufikia lengo la angalau asilimia 40 ya watu wenye ajira ifikapo mwaka 2020” alisema Dkt. Chuwa.Aidha Dkt. Chuwa alisema Ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Vijana, Ajira na wenye ulemavu na Shirika la Kazi Duniani (ILO) imeshakamilisha maandalizi yote ya kufanyika kwa utafiti huo, unaotarajia kuanzia katika Mkoa wa Dar es Salaam Mwezi Agosti hadi Novemba mwaka huu.Dkt. Chuwa alisema muundo wa utafiti huo umegawanyika katika ngazi kuu mbili, ikiwemo ngazi ya ukusanyaji wa taarifa katika ngazi ya kaya na ngazi ya pili ni ngazi ya biashara (uchumi), ambapo katika ngazi ya kaya, utafiti huo umejikita katika maeneo ya taarifa za kidemokrasia, elimu, hali ya ulemavu, ajira, ukosefu wa ajira.Akifafanua zaidi, Dkt. Chuwa alisema sampuli ya utafiti huo katika ngazi ya kaya pia utahusisha maeneo ya kuhesabia yapatayo 200 yaliyo mkoani Dar es Salaam na kaya zilizochaguliwa zaidi ya 2,400 pamoja na ukusanyaji wa taarifa kutoka kwenye biashara zaidi ya 4,000 na matokeo ya utafiti huo yatawezesha upatikanaji wa taarifa za kitakwimu ambazo ni wakilishi katika ngazi za Wilaya zote za Mkoa wa Dar es Salaam.MWISHO
↧
WAMETISHA
WINFRIDA MTOI
WAMETISHA, yeyote anaweza kusema hivyo kutokana na mambo
mawili yaliyotokea jana kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, wakati Yanga
ilipohitimisha tukio lao la Wiki ya Wananchi kwa mechi ya kirafiki dhidi ya
Kariobang Sharks ya Kenya.
Katika mchezo huo ulioambatana na utambulisho wa
wachezaji wapya, uliohudhuriwa na wapenzi, viongozi mbalimbali wa vyama,
serikali na wale wa Yanga, timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1.
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Harrison
Mwakyembe, ndiye aliyekuwa mgeni rasmi, akiambatana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es
Salaam, Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Ally Hapi na wengineo.
Mbali ya matokeo hayo, mashabiki wa Yanga walijitokeza
kwa wingi mno kiasi cha kuufunika Uwanja wa Taifa ili kuwashuhudia wachezaji
wao wapya ambao tangu wamesajiliwa, walikuwa wakiishia kuwasoma au kuwaona
kupitia vyombo vya habari.
Ikumbukwe kuwa msimu uliopita, wapenzi wengi wa Yanga
walionekana kutokuwa na mzuka na timu yao kutokana na usajili wa ‘kuungaunga
uliosababishwa na ukata.
Katika kuthibitisha hilo, kuna wakati pamoja na timu yao
kuongoza msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, bado walikuwa hawana amani,
wakiishia kuitazama ikicheza kupitia runinga.
Hata katika mchezo dhidi ya watani wao wa jadi, Simba,
waliojitokeza uwanjani walikuwa ni wachache mno tofauti na wenzao wa Msimbazi
ambao walifurika kwa wingi mno.
Na kwa hali iliyojionyesha jana, ni wazi safari hii
wapenzi wa Yanga wameonekana kuwa na imani na usajili uliofanywa na viongozi
wao, wakiliachia kazi benchi la ufundi kuwaunganisha wachezaji na kuwapa mbinu
na ujuzi kuunda jeshi la maangamizi.
Ukiachana na hilo la mahudhurio, kwa kiasi fulani usajili
mpya uliofanywa na Yanga umeonekana kuwaridhisha mashabiki, wakiamini safari
hii wana timu hasa.
Pamoja na sare waliyopata dhidi ya Kariobang Sharks
ambayo hivi karibuni iliichapa Everton ya England, lakini mashabiki wa Yanga
wametoka uwanjani jana wakiwa roho kwatu baada ya kuwaona wachezaji wao wengi
wapya wakicheza.
Kati ya wachezaji walioonekana kuwakosha wapenzi wa Yanga
jana ni washambuliaji Patrick Sibomana, Juma Balinya, Sadney Urikhob, lakini
pia kiungo Mapinduzi Balama na mabeki Mustapha Seleman, Lamine Moro, Muharami
Issa ‘Marcelo’, Ally Mtoni ‘Sonso’.
Pia, wengine wapya ambao walicheza ni washambuliaji
Maybin Kalengo na David Molinga ambao waliingia dakika za mwisho na hivyo
kukosa muda mzuri wa kuonyesha makali yao kama ilivyokuwa kwa wenzao hao.
Kati ya wote hao, kipa Farouk Shikalo ndiye aliyeonekana
kuwakosha zaidi wapenzi wa Yanga kwa umahiri wake aliouonyesha golini, akiokoa
mipira ya hatari.
Akizungumzia mchezo huo na viwango vya wachezaji wake,
Kocha Mkuu wa Yanga, Mwinyi Zahera, alisema kuwa ameridhishwa na kila
kilichotokea uwanjani jana, akiahidi kikosi chake kuwa moto zaidi ndani ya siku
15.
Alisema amefarijika na uwezo wa kila mchezaji akiamini
kuna mambo madogo madogo ambayo akiyafanyia kazi ndani ya siku hizo, kikosi
chake kitatisha msimu ujao.
“Tuna timu nzuri, nimewaona wachezaji walivyocheza na
uwezo wao, mashabiki wa Yanga wanipe siku 15 niisuke timu yao, wenyewe
wataipenda zaidi,” alisema Zahera.
Kwa upande wa mchezo huo wa jana, Yanga walipata kipimo kizuri kutoka
kwa Kariobang Sharks, wanaocheza soka la kasi na la kiufundi, wakiwa wamekaa
pamoja kwa muda mrefu tofauti na Wanajangwani wanaosuka upya ‘chama’ lao.
Yanga ndio waliokuwa wa kwanza kulifikia lango la wapinzani wao hao
ambapo dakika ya saba, beki wa kulia, Seleman alipiga krosi murua iliyotua kwa
Balinya, lakini beki wa Sharks, aliwahi na kuokoa hatari hiyo iliyozaa kona
tasa.
Dakika ya 11, Sadney alikosa bao baada ya kupokea pasi ya Mohammed Issa
‘Banka’, baada ya shuti lake kutoka pembeni ya lango.
Dakika moja baadaye, Balinya alipiga shuti kali ambapo kipa wa
Kariobangi Shanks, Brian Bwire, aliugusa na kutoka nje na kuzaa kona butu.
Yanga iliendelea kulishambulia lango la wapinzani wao hao ambapo dakika
ya 18, Sadney alipata pasi ya Sibomana, lakini alipiga shuti lililotoka
pembeni, huku dakika ya 22, Balinya akikosa bao, akiwa ndani ya boksi kutokana
na krosi ya Marcelo.
Kariobang Sharks walijibu mapigo ambapo dakika 27, Patrick Ngunyi
alikosa bao baada ya kuzidiwa maarifa na kipa wa Yanga, Shikalo, wakati
mshambuliaji huyo alipotaka kumpiga chenga ‘nyanda’ huyo.
Dakika ya 31, Balinya alipiga shuti kali lililogonga mwamba baada ya
kupata pasi ya Sibomana ambapo mpira uliporudi, ulimkuta Papy Tshishimbi aliyepaza.
Kipindi cha pili, Kariobang Sharks waliingia uwanjani kwa kasi na kupata
bao dakika ya 48 kupitia kwa Patrick Otieno, baada ya kupata pasi ya Harrison
Mwendwa.
Yanga walisawazisha bao hilo dakika ya 58, kupitia kwa Sibomana aliyeukwamisha
nyavuni mpira kwa mkwaju wa penalti iliyopatikana baada ya Sadney ‘kumnawisha’
beki wa Sharks, Samuel Qlwade.
Baada ya bao hilo, Yanga walicharuka kusaka lingine la ushindi, kama
ilivyokuwa kwa Sharks.
Balama aliikosesha Yanga bao baada ya kupaisha mpira akiwa ndani ya 18
kutokana na krosi ya Mrisho Ngasa.
Sadney aliyekuwa akiwasumbua mno mabeki wa Sharks, alikaribia kuipatia
Yanga bao la pili baada ya kuambaa na mpira hadi ndani ya sita, lakini shuti
lake likaokolewa na kipa Bwire na kuwa kona butu.
Dakika ya 87, David Simiyu wa Sharks, alikosa bao kwa kupiga mpira wa
kichwa nje akiwa yeye na kipa Shikalo, kabla ya Ngassa kushindwa kucheka na
nyavu dakika ya 90 baada ya shuti lake kutoka nje.
Kikosi cha Yanga: Farouk Shikalo, Mustapha Seleman, Muharami Issa
‘Marcelo’, Ally Mtoni ‘Sonso’, Lamine Moro, Mohammed Issa ‘Mo Banka’/Mrisho
Ngassa (dk64), Mapinduzi Balama, Papy Tshishimbi, Sadney Urikhob/David Molinga
(dk88), Juma Balinya/ Maybin Kalengo (dk 84) na Patrick Sibomana.
Kariobangi Shaks: Brian Bwire, Erick Juma, Samuel Qlwande, Kyata Amani,
Nixon Omondi, Yidah Sven, Shaphan Oyugi, Harrison Mwendwa, Patrick
Otieno/Julius Masaba (dk55), Patrick Ngunyi/James Mazembe (dk59) na Erick
Kapaito.
Katika hatua nyingine, viongozi wa timu ya Township Rollers ya Botswana,
walikuwapo uwanjani jana kuisoma Yanga, watakayokutana nayo katika mchezo wa
hatua ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika mwishoni mwa wiki hii jijini Dar es
Salaam.
↧
↧
Kenya: Msomi mwenye shahada sita afariki bila ajira
Familia ya msomi huyo sasa inatoa wito kwa wahisani kuisaidia kuchangisha dola 1,274 kugharamia mazishi yake.
↧
Gari ya Mkuu wa Mkoa wa Mara Adam Malima Yapata Ajali Likidaiwa Kuendeshwa na mtu anayedaiwa kuwa ni mtoto wa dereva
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Juma Ndaki amesema gari la mkuu wa Mkoa huo, Adam Malima limepata ajali jana Jumapili Agosti 4, 2019 likiwa linaendeshwa na mtu anayedaiwa kuwa ni mtoto wa dereva wa mkuu huyo wa Mkoa.Ndaki amesema ajali hiyo imetokea jana saa 3 asubuhi na kwamba gari hilo lenye namba za usajili STL 5961 lilikuwa likiendeshwa na mtu ambaye taarifa za awali zinaeleza kuwa ni kijana wa dereva wa Malima."Mtoto na Baba yake wote wamelazwa Hospitali, Mtoto ana majeraha baada ya kupata ajali na gari ya Mkuu wa Mkoa na huyu baba ambaye ni Dereva wa Mkuu wa Mkoa alianguka kwa Presha tukamkimbiza Hospitali, maana alipata mshtuko bada ya kufika eneo la tukio na kuiona ajali"-Amesema
↧
Mashambulizi mawili ya risasi Ohaio na Texas Nchini Marekani yaua watu 30
Watu kumi wameuawa kufuatia shambulizi la risasi katika mji wa Dayton, Ohio nchini Marekani. Polisi wamesema hayo mapema jana Jumapili na kuongeza kuwa mshambuliaj ni miongoni mwa waliouawa. Watu wasiopungua 16 wamejeruhiwa na wamepelekwa katika hospitali mbaimbali kwa matibabu. Shambulizi hilo linajiri katika muda wa saa 24, baada ya kutokea mkasa mwengine kama huo ambapo watu 20 waliuawa na 26 kujeruhiwa kwa kufyatuliwa risasi na mtu aliyekuwa na bunduki ndani ya duka moja kubwa eneo la El Paso, Texas. Polisi wamemkamata mwanaume anayeshukiwa kuhusika kwenye shambulizi la Texas mwenye umri miaka 21.Msemaji wa polisi wa El Paso Robert Gomez ameeleza kuwa wengi wa wahanga katika kisa cha Texas walimiminiwa risasi katika duka la Walmart. Gomez ameongeza kuwa wakati wa tukio hilo kulikuwa na karibu wateja 3000 kwenye duka. Polisi wamesema huenda shambulizi hilo lilichochewa na chuki za ubaguzi wa rangi. Jumla ya watu 30 wameuawa kwenye mashambulizi hayo mawili.
↧
Hivi ndivyo Wiki ya Mwananchi Yanga ilivyohitimishwa
KLABU ya Yanga
jana, ilihitimisha tamasha lake la Wiki ya Mwananchi, kwa kikosi cha timu hiyo
kulazimishwa sare ya bao 1-1 na Kariobangi Sharks ya Ligi Kuu Kenya, katika
mchezo wa kirafiki uliochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Timu hizo
zilikamilisha dakika 45 za kwanza zikiwa nguvu sawa.
Kwa ujumla, kipindi
cha kwanza, timu hizo zilifanya mashambulizi ya kupokezana.
Yanga
ilionekana vizuri katika umiliki wa mpira, lakini udhaifu ulikuwa katika kutengeneza
nafasi za mwisho ambazo zimeweka kuwapa mabao.
Hali hiyo
inaweza kuwa, ilichangiwa na ugeni wa wachezaji wachezaji wake wengi katika
kikosi cha timu hiyo.
Kwa nyakati
tofauti, wachezaji Sadney Urikhob, Juma
Balinya, Papy Tshishimbi na Patrick Sibomana walipoteza nafasi nzuri za kuipa
uongozi Yanga kipindi cha kwanza.
Kwa upande
wa Kariobangi, Patrick Ngunyi alishindwa
kutumia nafasi kuifungia bao.
Kipindi cha pili, kilipoanza Kariobangi iliingia na mkakati mpya na kufanikiwa
kuandika bao la kuongoza dakika ya 48 kupitia kwa Patrick Otieno kwa mkwaju
mkali, baada ya mabeki wa Yanga kuchelewa kumdhibiti akiwa ndani ya eneo la
hatari.
Bao hilo, halikuipunguza
nguvu Yanga, badala yake ilizidisha mashambulizi kwa lengo la kugomboa.
Dakika ya
56, mwamuzi wa mchezo huo Elly Sasii aliizawadia penalti Yanga, baada ya
mchezaji wa Kariobang, Shefan Oyug, kuunawa mpira ndani ya eneo la hatari.
Penalti hiyo
ilipigwa na Sibomana dakika ya 57 na kufungia Yanga bao la kusawazish.
Bao hilo ni
kama liliiongezea Yanga ari ya kupambana kwani ilizidisha kasi ya kulisakama
lango la Kariobangi.
Dakika ya
65, Yanga ilifanya mabadiliko alitoka Mohamed Issa na kuingia Mrisho Ngassa.
Pia ilifanya
mabadiliko mengine dakika ya 83, ambapo alitoka Balinya na kuingia Maybin Kalengo,
huku Kariobangi ikimbadilisha Erick Kapaito na kuingia David Simiyu.
Ili kuwapima
zaidi wachezaji wake, Kocha wa Yanga, Mwinyi Zahera alifanya mabadiliko dakika
ya 87, alitoka Urikhob na kuingia David Molinga.
Pamoja na
mabadiliko hayo yaliyofanywa na kila upande, dakika 90 zilikamilika kwa timu
hizo kufungana bao 1-1.
Kabla ya
mchezo huo, yalitanguliwa na matukio mengine likiwemo la utambulisho wa
wachezaji watakaoitumikia Yanga msimu ujao wa Ligi Kuu na mashindano mengine
ikiwemo Ligi ya Mabingwa Afrika.
Wampa jezi Rais Magufuli
Mwenyekiti
wa Yanga, Dk Mshindo Msolla pia alikabidhi zawadi ya jezi kwa Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli.
Jezi hiyo
ilipokelewa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison
Mwakyembe.
Mwisho wa
machungu
Dk Msolla alisema kutokana na mikakati ambayo wameifanya ndani ya Klabu
ya Yanga, wanachama hawatajutia tena kama msimu uliyopita.
Alisema, mipango yao ni mikubwa na
mpaka sasa wamekamilisha asilimia 80 ikiwemo pamoja na usajili kabambe ambao
wameufanya.
“Yanga hii mpya sio ya kubahatisha bali mambo mengi yanafanyika
kisomi,”alisema Dk Msola.
Alisema ili kuhakikisha kila jambo
linakwenda sawa, atahakikisha mipango
inakuwa kwenye mfumo na hakuna mali yoyote ya klabu itakayotumika bila
kutambulika.
Makambo
kusahaulika
Naye Makamu
Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga, Fredrick Mwakalebela alisema kwa namna ambavyo
amefuatilia video za nyota wao mpya, raia wa DRC, David Molinga, mashabiki wa
klabu hiyo watamsahau aliyekua straika wao , Eritier Makambo.
Alisema, awali
walitegemea nafasi hiyo ingezibwa na Mganda Juma Balinya, lakini Molinga mbadala
sahihi zaidi wa Makambo.
“Siwezi kumsemea sana kwa vile wananchi
hawajamuona lakini hiki ni kisu hatari, kitafunga mabao mengi sana, chamsingi tusubiri
tuone kazi yake,” alisema Mwakalebela.
↧
↧
Mzee wa miaka 95 aliyeombwa rushwa na polisi kumuona Magufuli
Abdallah Amiri-Igunga
MKAZI wa Kijiji cha
Isakamaliwa Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Ngaka Mataluma (95) na viongozi wa
CCM wa kata hiyo, wamepanga kuanza safari ya kwenda kuonana Rais Dk. John
Magufuli ili kushinikiza askari polisi sita wanaodaiwa kumuomba rushwa
wachukuliwa hatua za kisheria.
AskAri hao, ambao
wanadaiwa kuomba na kupokea rushwa ya Sh milioni 8 kutoka kwa Matalamu,
hawajachukuliwa hatua zozote na wakubwa zao, licha ya ushahidi kuwapo.
Akizungumza na MTANZANIA
nyumbani kwake mjini hapa juzi kwa niaba ya wenzake, Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji
cha Isakamaliwa Simon Makolo, alisema wamefikia uamuzi huo baada ya kuona
vyombo vya dola vimeshindwa kuchukua hatua stahiki.
Alisema wamepanga kuanza
safari ya kuonana na Rais Dk. Magufuli wakati wowote kuanzia sasa ili kufikisha
kilio chao.
“Wananchi wa Isakamaliwa, tumekuwa tukijiuliza
juu ya ukimya uliopo wa askari hawa na viongozi wawili wa Serikali ya Kijiji
cha Isakamaliwa, wanaotuhumiwa kuomba na kupokea rushwa ya shilingi milioni nane
kutoka kwa Mataluma kutofikishwa mahakamani.
“Hali imesababisha
Mataluma na viongozi wenzangu, tujipange kwa safari ya kwenda kuonana na rais,
tukiamini atatusaidia jambo hili ili haki itendeke,”alisema
Alisema amekuwa
akisumbuliwa na wananchi na Mataluma mwenyewe kutokana na kesi hiyo
kutofikishwa mahakamani tangu Juni 12, mwaka huu, lilipotokea tukio hilo.
Alisema yeye na viongozi
wengine, walitoa maelezo yao kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa
(TAKUKURU) na jeshi la polisi.
Alisema katika safari
hiyo, Mataluma atafuatana na Mwenyekiti
wa CCM tawi la Isakamaliwa, Nkwabi Galishi na mkazi wa kijiji hicho, Jilunga
Mwangali, viongozi wawili, mmoja wa serikali ya kijiji na mmoja wa chama ambaye
ni katibu wa tawi na mfanyabiashara
aliyenunua ng’ombe 11.
Alisema pamoja na hatua
hiyo, Mataluma amekuwa akisumbuliwa na mfanyabiashara Kashinje Mhela aliyenunua
ng’ombe wake 11 ambao alilazimishwa na polisi hao akitaka arudishwe fedha zake
Sh milioni 8.
“Ukimwangalia yule mzee
Mataluma amezeeka kweli kweli, sasa anasumbuliwa na huyu mfanyabiashara
arudishiwe fedha zake shilingi milioni 8 ambazo zinadaiwa kuchukuliwa na hawa
askari. Anaishi maisha ya hofu kila kukicha, jambo hili lazima lipate ufumbuzi,”alisema.
UHAMISHO
Pamoja na kilio cha
Mataluma, kuna taarifa za uhakika kutoka vyanzo vya jeshi la polisi Igunga,
kuwa askari wamehamishwa vituo vingine vya kazi katika wilaya za Sikonge, Uyui
na Nzega.
Inaelezwa Inspekta Frank
Matiku (36) ambaye aliongoza askari hao kwa kile kichodaiwa rushwa, amehamishiwa
Wilaya ya Sikonge kuwa Mkuu wa Upelelezi Msaidizi, PC Raphael Maloji (31) na Koplo
Paulo Bushishi (49), wanahamishiwa Wilaya ya Uyui, DC Lucas Nyoni (31), PC Lome
Laizer (39) na Koplo Charles Zacharia (45), wamehamishiwa Wilaya ya Nzega.
Mkuu wa Wilaya ya Igunga,
John Mwaipopo alipoulizwa juu uhamisho huo jana, alisema yeye hajapata taarifa
yoyote.
Kwa upande wake, Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Tabora, Barnabas Mwakalukwa alipoulizwa alisema hana taarifa hizo.
“Umezipata taarifa hizi wapi,
mimi ndio naingia Tabora, nitafuatilia,” alisema Mwakalukwa.
Hivi karibuni, Mkuu wa Takukuru
Mkoa wa Tabora, Chaulo Mussa alisema wanasubiri askari hao wafukuzwe kazi na mwajiri wao ili wawafikishe mahakamani.
Juni 12, mwaka huu katika Kijiji
cha Isakamaliwa, askari hao na Mwenyekiti wa Kitongoji cha Zahanati, Juma
Mwagala na Ofisa Mtendaji wa Kijiji chicho, Edward Kitenya walituhumiwa kuomba
na kupokea rushwa ya milioni 8 kutoka
kwa Mataluma, wakimtuhumu kujihusisha na vitendo vya upigaji ramli chonganishi,
kumiliki nyara za serikali, zikiwamo ngozi ya kenge na bunduki aina ya gobole.
↧
Simanzi yatawala mazishi aliyechomwa na mume wake
Andrew Msechu-DAR ES SALAAM
NI simanzi. Ndivyo unaweza kusema,baada ya
mamia ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, kukusanyika na kushiriki mazishi ya
Naomi Marijani, ambaye anadaiwa kuuawa na mume wake, Khamisi Luwongo, kisha
kuteketeza mwili wake kwa kuuchoma moto.
Inadaiwa Naomi, alitoweka katika mazingira
ya kutatanisha Mei, mwaka huu, ambapo picha na taarifa zilizodaiwa kuandaliwa
na mumewe Luwongo, zilisambazwa kwenye mitandao ya kijamii zikidai
atakayefanikisha kupatikana kwake, atapa zawadi ya Sh milioni moja.
Kutokana na taarifa hizo ambazo baadaye,
Kamanda Polisi Mkoa wa Kipolisi Temeke, Amon Kakwale, alisema Mei 19, mwaka huu, Luwongo alifika
katika Kituo cha Polisi Gezaulole, Kigamboni na kufungua jalada la taarifa kuwa
mkewe, Naomi ametoroka.
Alisema kama ilivyo taratibu za polisi,
walianza uchunguzi na Juni 12, Luwongo
alifika tena kituoni hapo na kueleza kuwa
mke wake, ametelekeza mtoto wao anayeitwa Grecious (7).
Jana ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu
Naomi, walikusanyika nyumbani kwa kaka yake Mbweni, Dar es Salaam na kufanya
ibada wa mazishi kama ishara ya kutimisha msiba wake.
Katika ibada hiyo, pia ilihudhuriwa na
majirani wa Naomi waliokuwa wakiishi naye Kigamboni pamoja na vikundi
mbalimbali vya kwaya.
Akizungumza wakati wa ibada hiyo ya
mazishi, Mchungaji wa Kanisa alilokuwa akisali marehemu Naomi la Sabato Gezaulole, Jackob Chimbwegu, alisema wakati wote wa uhai
wake marehemu alikuwa mshirika mzuri ambaye alisababisha kununuliwa kwa viti
vya kisasa plastiki.
“Tumeguswa sote, kwa kilio cha maumivu
mliyonayo ndugu, hakuna namna ya kuwatuliza. Zaidi ni kumwomba Mungu awatulize
mnaopita katika wakati huu mgumu,” alisema Mchungaji Chibwengu
Pamoja na hali hiyo, aliwataka
waombolezaji kujiweka tayari kuonana na Mungu kwa kuwa katika maisha ya
binadamu ni mafunzo tosha, kwani hakuna anayejua atakavyoondoka hapa duniani.
Naye Mchungaji Emmanuel Mhando wa Kanisa
la FPCT, alisema kuna maswali mengi watu wanaweza kujiuliza, kwa nini Naomi,
kwa nini kifo kiwe cha namna hii?
Alisema kwanini zinakuwa nyingi, lakini hakuna
haja ya kulalamika tena, hakuna haja ya kujiuliza, bali kuomba nguvu ya kusonga
mbele.
“Ni imani yangu baada ya ibada hii,
tusiendelee kulaumu, tuseme inatosha, inatosha, tumuombe Mungu atupe nguvu ya
kusonga mbele,” alisema Mchungaji Mhando
KAULI YA FAMILIA
Kwa upande wake,msemaji wa familia,
Wiseman Marijani alisema jambo lililowasibu ni zito na gumu wakati wote
walikuwa wamezongwa na hawakujua nini cha kufanya.
Alisema familia inapenda kumshukuru Mungu
kwa mambo makuu, tangu Naomi aliyedaiwa
kupotea Mei 15, mwaka huu, lakini wakaja kujua aliko siku 60 baadaye.
“Tulianza kukata tama, Mungu alitufungulia
fumbo na kujua aliko Naomi, baada ya mbingu kumlazimisha Meshack, mumewe
kueleza kinagaubaga kuhusu ukatili alioufanya, alisema.
Alisema anaushukuru uongozi wa Wizara ya
Mambo ya Ndani ya Nchi na Jeshi la Polisi, vyombo vya habari pamoja na wananchi
ambao walisaidia kupata taarifa za haki aliko Naomi.
Alisema taarifa zilizosaidia kujulikana
aliko Naomi zilipatina kutoka kwa msamaria ambaye aliwapa mbinu iliyosaidia
kutanzua fumbo hilo
Alisema kwa kuwa suala hilo liko
mahakamani, wanaiombea mahakama iweze kutoa haki stahiki.
Alisema baada ya ibada maalumu kufanyika
jana, familia itaendelea kusubiri mamlaka husika ili ziwarejeshee mabaki ya
mwili wa Naomi ili waweze kumpumzisha kwa amani.
TAARIFA ZA KUUAWA
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa
Kipolisi Temeke, Amon Kakwale alisema baada ya utata wa taarifa za tukio hilo,
polisi walianza utaratibu wa uchunguzi
ambapo Juni 12, Luwongo alifika tena kituo hicho cha polisi na kueleza
kuwa Naomi ametelekeza mtoto anayeitwa Grecious mwenye umri wa miaka saba.
Kamanda huyo alisema baada ya Jeshi la
Polisi kupokea taarifa hizo, kesi hizo zilianza kufanyiwa kazi.
Alisema wakati wanaendelea na uchunguzi
juu ya suala hilo, ndugu wa Naomi nao walifika katika kituo cha Polisi
Chang’ombe, wakieleza kuwa ndugu yao alikuwa amepotea na wana shaka na mumewe
kuhusu kutoweka kwake.
Alisema kutokana na maelezo hayo ya ndugu
wa Naomi, Jeshi la Polisi likamtia mbaroni Luwongo kwa ajili ya mahojiano.
Alisema Julai 15, akiwa mbele ya jeshi
hilo akaeleza taarifa alizokuwa ameeleza awali hazikuwa za kweli na akaanza
kueleza ukweli wa namna mkasa mzima ulivyokuwa.
Julao 30, mwaka huu, mume aliyekuwa
akishikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kumuua mkewe, kisha kumchoma kwa
mkaa magunia mawili ya mkaa na kumzika shambani kwake, Khamisi Luwongo
(Meshack), alifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kusomewa mashtaka
yanayomkabili.
Luwongo, alifikishwa mahakamani hapo na
kuwekwa mahabusu ya mahakama hiyo akisubiri kupangiwa Hakimu.
Hata hivyo, jalada la kesi ya mauaji ya kukusudia limepangwa kusikilizwa
mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustine Mmbando.
Mshtakiwa anatuhumiwa kumuua mkewe Naomi (36), Mei mwaka
huu katika maeneo ya Kigamboni,Dar es Salaam.
↧
TAMASHA la tatu la Utalii na Michezo lafikia tamati
KIJANA Ali Khamis Abdalla akiwa nje ya gari yake baada ya kuibuka mshindi wa kwanza katika bonanza la Utalii, lililofikia tamati katika fukwe za Vumawimbi Wilaya ya Micheweni.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA) KIJANA Ali Khamis Abdalla (Wanne katika picha) Kutoka Tumbe Wilaya ya Micheweni, ambaye ameweza kujinyakulia Gari yenye Thamani ya Milioni 7 baada ya kuibuka mshindi wa kwanza katika mashindano ya Traithoni, ikiwa ni bonanza la Tatu utalii Kisiwani Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA) KIJANA Ali Khamis Abdalla akiwa ambaye ni mshindi wa kwanza katika bonanza la utalii Pemba(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)GARI ambayo amekabidhiwa bingwa wa bonza la utalii Kiswani Pemba(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)NA ABDI SULEIMAN NA SAID ABDURAHMAN, PEMBA.TAMASHA la tatu la Utalii na Michezo Kisiwani Pemba, limefikia tamati kwa michezo mbali mbali ikiwemo trithon, mchezo wa kuogolea na resi za ngalawa, huko katika fukwe za vumawimbi wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kusini Pemba.Mtamasha hilo liliweza kuvuta hisia za mashabiki wengi katika kisiwa hicho, hali iliyopelekea kuujaza ufukwe wa vumawimbi, huku likiwashirikisha wanamichezo wapatao 500 kutoka Zanzibar na Tanzania bara.Baadhi ya wananchi wa wilaya ya micheweni walishindwa kuzuwia hisia zao, baada ya kumuona kijana wao Ali Khamis Abdalla kutoka Tumbe, kuongoza katika mbio za baskeli na kujinyakulia gari, huku wakishindwa kuamini kilichotokea.Tamasha hilo ambalo limefungwa na Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mgeni Hassan Juma, ambapo washindi mbali mbali waliweza kuzawadiwa zawadi Washindi hao waliweza kuzawadi mbali mbali zikiwemo fedha taslimu, baskeli, Honda aina ya boxer na sunlj, huku mshindi wa mashindano hayo akijinyakulia Gari.Kwa upande wa michezo ambayo ilishindaniwa na kutolewa zawadi katika ufungaji huo, ni pamoja na resi za baskeli, mpira wa miguu, resi za ngawala, uogeleaji, dufu pamoja na mbio za trithon.Kwa upande mbio za trithon ambazo ziliwashirikisha vijana kutoka Unguja na Pemba, zikiwashirikisha washiriki 51, ambapo mshindi wa Kwanza ni kijana Ali Khamis Abdalla kutoka Tumbe Wilaya ya Micheweni, alijinyakulia gari aina Vtz pamoja na kikombe. Mshindi wa pili wa mbio hizo ni Khamis Juma Khamis kutoka Dimani Unguja, ambapo yeye alijinyakulia Honda huku nafasi ya tatu ilichukuliwa na kijana Hassan Ame Tajo kutoka Dimani nae akajinyakulia Honda aina boxer, huku washiriki 10 wa mwanzo wakiahidiwa kila mmoja kuzawadiwa shilingi 50,000/.Kwa upande upigaji dufu, mshindi wa Kwanza kilikuwa ni chuo Cha Almadrasatul Nurul-Islamiyya kutoka Micheweni ambapo kimejinyakulia kitita Cha shilingi 3000,000/ taslimu, nafasi ya pili ikichukuliwa na Almadrasatul Munir Islamiyya kutoka Kangani Mkoani Pemba ambapo nacho kikajinyakulia kitita Cha shilingi 2000,000/ huku nafasi ya tatu ilichukuliwa na Almadrasatul Thamaratul Jannar ya Fundo ikajipatia shilingi 1000,000/ huku walimu wa madrasa hizo walizawadiwa baskeli kila mmoja.Kwa upande wa Mashindano ya uogeleaji mshindi wa Kwanza alikuwa ni Hamad Mattar Abdalla ambae alijinyakulia kitita Cha shilingi 1000,000/ pamoja na kikombe, mshindi wa pili ni Faki Omar Faki nae akajinyakulia shilingi 700,000/ na mshindi wa tatu alikuwa ni Ali Hamad Shaame akijichukulia kitita Cha shilingi 500,000/, ambapo katika mchezo huo waogoleaji wapatao 71 walishiriki Mashindano hayo.Ama kwa upande resi za ngalawa zilizoshirikisha ngalawa 12, nafasi ya kwanza ikichukuliwa na Simba Salim Issa kutoka Mnarani Makangale ambae alijipatia kitita Cha shilingi 1000,000/ na kikombe, nafasi ya pili ikichukuliwa na Said Khamis Rashid alijipatia kitita Cha shilingi 700,000/ na mshindi wa tatu ni Ali Shaame kutoka Mnarani akajinyakulia shilingi 500,000/ huku washiriki waliosalia wakiahidiwa shilingi 100,000/.Kwa upande wa mbio za marathon upande wa wanaume nafasi ya kwanza ilichukuliwa na kijana Nelson Mbuya kutoka JKU ambae alijipatia kitita Cha shilingi 800,000/, nafasi ya pili ikachukuliwa na Ali Malik Mohammed na kujinyakulia shilingi 700,000/ na nafasi ya tatu ilichukuliwa na Mohammed Ramadhani Mgeni kutoka KMKM ambae alijipatia kitita Cha shilingi 400,000/.Kwa wanawake ambapo washiriki walikuwa ni wawili tu mshindi wa Kwanza alikuwa ni Rosemary Gusta kutoka KMKM, ambae alijipatia kitita Cha shilingi 400,000/, huku nafasi iliyosalia ikichukuliwa na Asha Abdalla Khatib ambae na akipata shilingi 300,000/.Kwa upande wa mchezo wa mpira wa miguu ambayo ilishirikisha vilabu 8 vya mchezo huo, mshindi ilikuwa ni timu ya Mwenge kutoka Wete, ilijipatia kikombe pamoja na fedha taslim shilingi 3000,000/, mshindi wa pili akizawadiwa fedha taslim shilingi 2000,000/, huku vilabu vilivyobakia wakiahidiwa mipira ya kuchezea kila timu.Akitoa nasaha zake Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mgeni Hassan Juma, alisema Zanzibar ilikuwa na ndoto ya kuanzisha mashindano ya trithon jambo ambalo sasa limetimia kwa upande wa Kisiwa Cha Pemba.Alisema kufanyikwa mashindano hayo ni kielelezo tosha cha kuibua vipaji vya wachezaji mbali mbali ya vijana, hali ambayo inaweza kuhamasisha vijana kujiingiza katika sekta ya utalii.“Kwa sasa michezo ni ajira na imekuwa ikiajiri vijana wengi na kutoka sehemu mbali mbali duniani, hivyo vijana kutumia nafasi hii ya michezo kujitangaza kwenu”alisema.Tamasha hilo ambalo lilifunguliwa rasmi na Rais Mtaafu wa awamu ya pili wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Alhaj Ali Hassan Mwinyi mwishoni mwa wiki iliyopita, ambapo hapo Jana limefungwa na Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Mgeni Hassan Juma, michezo mbali mbali iliweza kufanyika.
↧