KIPUTE cha michuano ya kimataifa kinatarajia kuanza mwishoni mwa wiki hii kwa Ligi ya Mabingwa na Kombe la Shirikisho kwa wawakilishi wetu wanne kuanza kutupa karata zao uwanjani huku Yanga pekee ikianzia nyumbani.
↧
Mastaa hawa kuzibeba timu michuano ya Caf
↧
Mechi hizi sio za kukosa FDL
Ni moto! Msimu mpya wa Ligi Daraja la Kwanza (FDL) unatarajiwa kuanza kurindima Septemba 14, ambapo timu 24 zilizopangwa katika makundi mawili zitakinukisha katika michuano hiyo kuwania nafasi ya kupanda Ligi Kuu Bara kwa msimu wa 2020-2021.
↧
↧
Ukuta wa chuma Man United
KOCHA wa Manchester City, Pep Guardiola amewapongeza mahasimu wao wa mji mmoja, Manchester United kwa kufanikisha dili la usajili wa Harry Maguire, huku akisema klabu yake “ilishindwa kumudu bei” ya beki huyo wa Leicester City.
↧
Madaktari wa Cuba waliotekwa Kenya na al-Shabab walazimishwa kusilimu
Vyanzo vya kiintelijensia nchini Kenya vinaashiria madaktari wawili wa Cuba waliotekwa nchini Kenya wamesilimishwa kwa lazima.
↧
Uhuru amweka Ruto kiporo urais 2022
ISIJI DOMINIC
SIASA za
kuelekea uchaguzi mkuu mwaka 2022 zinazidi kumchefua Rais wa Kenya, Uhuru
Kenyatta ambaye amekuwa akisisitiza wanasiasa kuwatumikia wananchi na kuacha
kupiga siasa hadi muda wa kampeni utakapofika.
Hata hivyo,
ushauri huu wa Rais Uhuru ni kama unapuuzwa na wanasiasa tena wale kutoka chama
tawala cha Jubilee ambao wanadai ni vigumu kutenganisha siasa na kuwatumikia
wananchi.
Kundi hili
ambalo wengi wanamuunga mkono Naibu Rais, William Ruto katika mbio za kuwania
urais 2022 wanasema jukumu la kwanza la mwanasiasa ni kupiga siasa kwa
kisingizio kuwa unaweza ukasahaulika kama hujihusishi na siasa ukisubiri muda
wa kampeni.
Hii ni hoja
ambayo wananchi wanapinga na kusisitiza mwanasiasa au kiongozi anayewatumikia
waliompigia kura kwa kuhakikisha anasimamia miradi ya maendeleo ndiye
atakayepata kura kutokana na kazi yake kuonekana kwa vitendo.
Rais Uhuru
ambaye anakerwa na baadhi ya wanasiasa ndani ya Jubilee wanaomshinikiza atamke
kumuunga mkono Ruto kama mrithi wake, hivi karibuni alitoa maneno ambayo
yanaashiria huenda asimuunge mkono naibu wake 2022.
Akizungumza Ruto
katika Kaunti ya Kiambu wakati anafungua kiwanda cha Bidco, Uhuru alisema ni
Mungu pekee ambaye ataamua nani atakuwa Rais ajaye hivyo kuwataka viongozi
kuacha kuweweseka na badala yake kuwahudumia Wakenya.
“Uchaguzi
utakuja na Mungu ndiye hupeana uongozi. Tufanye kazi,” alisema na kauli yake ilitafsiriwa
kumlenga Ruto ambaye amekuwa akizunguka maeneo mbalimbali nchini Kenya, ikitajwa
ni lengo la kujitambulisha huku wafuasi wake wakisema Rais Uhuru anatakiwa kutimiza
ahadi aliyotoa 2013 ambayo ni kumuunga mkono Naibu Rais.
Moja wa
wafuasi sugu wa Ruto, Oscar Sudi ambaye ni Mbunge wa Kapseret, alinukuliwa
akimtaka Rais Uhuru kujiuzulu akijigamba anaweza kuongoza nchi vizuri endapo Rais
atamuachia kwa miezi mitatu tu.
“Ukiona Rais
hawezi kukutana na viongozi, magavana na maseneta ambao wanalazimika kuandamana
barabarani, ujue iko shida,” alisema Sudi akiwa nyumbani kwake Kapseret, Kaunti
ya Uasin Gishu.
Kelele za
baadhi ya wanasiasa wa Jubilee zinazolenga kumpigia debe Naibu Rais Ruto
hususan baada ya kitendo cha Machi 9 mwaka jana, Rais Uhuru alipokutana na
kiongozi wa upinzani Raila Odinga na kuzika tofauti zao za kisiasa, zimekuwa zikizimwa
na Uhuru ambaye amepania kutimiza ajenda nne kuu ikiwemo kupambana na ufisadi.
Kauli ya
Rais Uhuru ya hivi karibuni kwamba Mungu ndiye hupeana uongozi ikionekana
kukwepa kumpigia debe Ruto inakinzana kwa kiasi fulani na ile aliyowahi kusema
mwaka jana akiwa ziarani Nyeri kufungua soko la Karatina.
Rais aliyeonekana
kukasirishwa na wabunge wanaoteka eneo lake la ubunge muda mwingi kutumia
kujadili siasa za 2022 badala ya kufanya mambo ya msingi yanayogusa wananchi,
alisema chaguo la mrithi wake litawashangaza wengi.
“Wanafikiri
kwa sababu Uhuru ataenda nyumbani 2022, hatakuwa na neno la kusema kuhusu nini
kitakachotokea. Ninawaambia wakati muda muafaka ukifika, nitakuwa na kitu cha
kuzungumza,”alisema Rais Uhuru katika mkutano wa hadhara.
“Wengine
wanafikiri nimenyamaza kwasababu siwezi kuongea kuhusu siasa. Mimi bado ni
mwanasiasa. Watashangaa chaguo langu muda huo utakapofika, lakini kwa sasa
nataka nijihusishe na kutekeleza ahadi nilizotoa kwa Wakenya.”
↧
↧
Kumpongeza Magufuli sio kosa, ni haki yake
MHINA SEMWENDA
KAMA kijana ninajiona
nina deni kubwa sana kwa nchi yangu, mimi kama Mtanzania nimebahatika
kushuhudia, ukuaji mkubwa wa nchi yetu katika awamu hii ya tano chini Rais Dk.
John Magufuli.
Nashukuru sana Mungu
amenijalia uhai wa kuweza kuona maendeleo haya.
Miaka ya nyuma kabisa
nikiwa chuo kikuu cha Dar es Salaam, niliwahi kutamani kumwona Magufuli akiwa
Rais, sidhani kama wakati huo yeye binafsi alikuwa na malengo ya kuwa Rais, hamasa
niliipata kutoka kwenye wimbo wa msanii Roma Mkatoliki enzi hizo sikuwahi kuhisi
kama Magufuli angekuwa Rais ila niliishia tu kutamani.
Nashukuru ndoto yangu
ilikuja kuwa kweli, na sasa yale niliyoyatamani ninayaona kwa macho yangu. Maeneo
mengi ya nchi yetu sasa yanapitia katika mabadiliko makubwa ya ujenzi wa
miundombinu ya barabara, madaraja, vituo vya kufua umeme, ujenzi wa shule na
hospitali pamoja na mengine mengi.
Kwa bahati mbaya,
sijawahi kuwa mwanasiasa wala sijawahi kutamani kuwa mwanasiasa lakini ni ukweli
usiopingika kwamba Rais Magufuli anafanya kazi nzuri.
Kwa dhati ya moyo wangu
nampongeza Rais Magufuli, hakika naamini na bado naamini kabisa kwa tulikopitia
watanzania na maendeleo yanayofanyika sasa. Sisi Watanzania tulipaswa kuwa wasemaji
wakuu wa huyu mzee na kupongeza jitihada zake.
Lakini kwa siasa za
Tanzania zilivyo, sasa Rais Magufuli anatumia nguvu kubwa kutueleza tena watanzania
kile anachotufanyia nahisi labda kuna wakati anataka kukata tamaa na nahisi
labda ndio namna siasa inavyomtaka afanye.
Kiubinadamu hata kama
unamfanyia mtu jambo kubwa na hakuelewi unaamua kuachana naye na kuendelea na
mambo yako. Ni sawa na mzazi anayepambana na mtoto ambaye hataki shule mwisho
wa siku mzazi akikata tamaa akamuacha mtoto ndio huwa anaharibikiwa.
Mara nyingi ukimsikiliza Rais
Magufuli anazungumza kuhusu Tanzania na maendeleo ya Tanzania kwa Watanzania
wenyewe akiitakia mema Tanzania, sasa hata kama ni siasa ndio zilivyo ifike
muda basi tumwelewe huyu mzee tumpe nafasi ya kuendelea kutufanyia kazi hii kubwa
anayoifanya.
Ninachokiona mimi sio
sawa Rais kutumia nguvu kubwa kutufanyia kazi halafu bado tena atumie nguvu
kubwa kutueleza kazi anayofanya kwa sababu anayoyafanya yanaonekana.
Mimi kama kijana
ninajiona nina deni kubwa kwa sababu sioni kama naitendea haki nchi yangu kwa
kushindwa kusimama na kuisemea, tukiachana na itikadi za kisiasa.
Vijana tunapaswa kuwa mstari
wa mbele kuyasema haya na kupongeza na kuwa mstari wa mbele, kuilinda nchi yetu
na rasilimali zetu huku tukiwaacha wanasiasa waendelee na siasa zao.
Sio kweli kwamba kazi
haifanyiki, inafanyika na tunaona sasa kwanini bado tena tunalaumu na
kulalamika au wakati mwingine na kutukana kabisa.
Mimi sio mwanasiasa kama
nilivyosema, lakini kila kijana au mtu akisimama na kusema au kutoa pongezi kwa
Serikali hii utasikia au utaambiwa unahitaji kupewa ukuu wa wilaya au ukurugenzi,
kitu ambacho sio sawa.
Lazima tujenge misingi ya
kutofautisha uzalendo wa kusifia maendeleo na uzalendo wa kuipenda Tanzania na
siasa au itikadi za chama kimoja au kingine.
Kupongeza au kusifia sio
kosa au sio dhambi, ni utashi tu wa kibinadamu. Sasa kama itikadi za kisiasa ndio
zinafanya tushindwe kuona yanayofanywa hata kama yanaonekana basi kuna shida
kwenye siasa zetu.
Muda wote ninaposhuhudia
siasa zetu nimejaribu kuwa muwazi ili nisiburuzwe na itikadi bali niwe katika
mtazamo wa wazi.
Kiubinadamu viongozi
wanaweza kukosea wao sio malaika lakini sio baya moja lifute mazuri yote
yaliyofanywa. Kila binadamu anafanya makosa hata mimi binafsi nimefanya makosa
huko nyuma na bado nitafanya makosa.
Iweje kila linalofanywa
kwa maendeleo ya nchi yetu lionekane baya kisiasa wakati kiuhalisia sisi ndio
tunaonufaika nalo?
Nitatoa mfano midogo,
ujenzi wa hospitali ni kwa manufaa yetu au wanasiasa? ujenzi wa barabara ni kwa
manufaa yetu au, ujenzi wa madaraja ni kwa manufaa yetu au? Jibu ni ndio kwa sababu
sisi ndio watumiaji wakuu wa miundombinu hiyo pamoja na mingine mingi.
Ubora wa barabara ni kwa
manufaa yetu pamoja na mengine mengi, sasa sijui watanzania tunatakiwa
tufanyiwe nini na viongozi wanaokuwa madarakani ili tuweze kuelewa na
kuwapongeza huku tukiweka itikadi zetu za kisiasa pembeni.
Tukiachana na sifa za
kisiasa au pongezi za kisiasa na wanasiasa, Watanzania tunapaswa kuwa wasemaji
wakuu wa maendeleo yetu kwa nchi yetu.
Na sio kuwaacha wanasiasa
kuwa wasemaji wa midomo yetu, kuona kwa macho yetu na kuhisi hisia zetu, kwamba kila atakayesifia
anataka madaraka au anataka kiki au anataka kujionesha hii sio sawa
kabisa.
Tujifunze kutengenisha
siasa na maendeleo ya nchi yetu. Tuiangalie nchi yetu kwanza kisha siasa ndio
zifuate. Siasa isiwe sehemu ya kukatisha tamaa, watendaji wa Serikali katika
kutimiza majukumu yao au siasa isiwe sehemu ya kuwafanya watanzania wasiwe huru
kusifia maendeleo wanayoyaona.
Mnyonge mnyongeni lakini
haki yake mpeni, Rais Magufuli anafanya kazi kubwa kwa nchi hii. Tumuunge mkono
na tuwe sehemu ya kumpa moyo na faraja ili apate moyo wa kufanya makubwa kwa
nchi yetu.
Kuna siku niliwahi kuwaza
jambo moja. Hivi mtu anapokuwa kiongozi (Rais) na akafanya kazi yake vizuri ana
lipi la kupoteza kati yetu sisi Watanzania au yeye kiongozi.
Nitatoa mfano, Rais wa
awamu ya nne, Jakaya Kikwete au Rais wa awamu ya tatu, Benjami Mkapa na Rais wa
awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi wana lipi la kupoteza?
Baada ya kumaliza vipindi
vyao na sasa wamepumzika. Hayo waliyoyafanya katika kipindi chao wasingeyafanya
kwani wasingekuwa walivyo sasa?
Wamefanya yao mengi
mazuri na mengine mabaya, lakini sasa wamepumzika wamemuachia kijiti Rais
Magufuli ambaye naye itafika siku yake atapumzika.
Sasa kwanini kwa haya
anayoyafanya kwetu sisi Watanzania tusimpongeze na kumpa moyo afanye zaidi
maana mwisho wa siku, sisi ndio wanufaika wa haya yote.
Vijana bado tuna deni
kubwa kuisimamia nchi yetu na kuuweka uzalendo wetu mbele na kuachwa kuongozwa
na itikadi za kisiasa, hata tukasahau mambo ya msingi katika kuijenga nchi
yetu.
Lazima tujenge utamaduni
wa kujivunia vilivyo vya kwetu. Rais ni wetu tulimchagua wenyewe kwanini
tusimuunge mkono na kumpa nguvu kuipeperusha bendera na nchi yetu vizuri?
Popote duniani, ukitamka
Tanzania lazima Magufuli ndio aonekane nyuma ya bendera yetu sasa kwanini
tusimuunge mkono na kumsaidia kuipaisha nchi yetu kimaendeleo.
Vijana tuna deni kubwa
kwa nchi yetu tusipoliangalia hili sijui, watoto wetu siku zijazo watakuwa na
hali gani.
Mimi binafsi nimejitoa
kukupongeza na kukusifia na zaidi kukutia moyo. Pambana. Nchi yetu itafika
tunakotaka. Mengineyo yatafuata baadaye.
Kwa sisi tusio wanasiasa
hatufuati itikadi zetu, lakini tunamsemea mama Tanzania ambaye wewe leo ndio
unamjenga na alama unazoweka zitabaki daima hata kama sio kwetu ni kwa watoto
wetu na wajukuu zetu.
mhina.semwenda@gmail.com
↧
Ukosefu wa shule ulivyoharibu ndoto za watoto Bagamoyo
*Dk. Kawambwa aomba wadau wa maendeleo kujitokeza
AVELINE KITOMARY
NI ukweli usiopingika kuwa elimu ni
msingi wa ustawi mzuri wa kutambua, kuelewa na kufanya vitu mbalimbali katika
kila jamii yoyote ile inayohitaji kusonga mbele kimaendeleo.
Katika jamii yetu, zamani ilikuwa
ikitolewa elimu ya mila,utamaduni na desturi mbalimbali ambapo wazee au wazazi
walijihusisha kuwapatia elimu watoto na vijana.
Lakini kwa ulimwengu wa sasa wa
ushindani ili nchi au sehemu yoyote iweze kufanikiwa kiuchumi,kisiasa, kilimo, ufugaji
na mengine kuna haja ya kupitia darasani kupata elimu.
Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage
Nyerere katika kipindi chake cha uongozi alipata kuwataja maadui watatu wa
maendeleo kuwa ni ujinga,maradhi na umasikini.
Muonekano wa kijiji cha Fuyosi, kitongoji cha Kalimeni, Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani
Kutokana na hilo, Rais wa awamu ya
tano, John Magufuli amefanikiwa kwa kiwango kikubwa kupambana na maadui hao.
Pamoja na mafanikio hayo, lakini kwa
baadhi ya sehemu kumekuwa na changamoto kubwa ya elimu,afya na umasikini.
Mwandishi wa makala hii ataelezea
jinsi ukosefu wa huduma za kijamii kama elimu unavyoangamiza ndoto za watoto
wengi katika Kijiji cha Fuyosi iliyopo Kitongoji cha Kalimeni wilayani Bagamoyo
katika Mkoa wa Pwani.
Kitongoji hicho cha Kalimeni kina
jumla ya kaya 268 ambapo kati yao kuna wanaume 144 na wanawake 124 takwimu hizo
ni za mwaka 2017 lakini bado kunaongezeko la watu.
Shughuli kubwa inayofanywa katika
kitongoji hicho ni kilimo cha mahindi na mihogo, hata hivyo wanakijiji hao
bado wako katika umasikini uliokithiri.
Asilimia kubwa ya
wanakijiji hawajui kusoma wala kuandika, kuanzia wakubwa mpaka wadogo,
naweza kusema hawaendani kabisa na dunia ya sasa ni kama watu waliosahaulika
gizani.
Umasikini na ukosefu wa huduma za
shule, afya,maji, migogoro ya wakulima na wafugaji na barabara, umekuwa ukizunguka
kingo za Kitongoji hicho tangu nchi ipate uhuru.
Kizazi hadi kizazi wamekuwa hawana
desturi ya kupata elimu, watoto wengi sasa wako kijijini bila hatima yao
kujulikana.
Kutokana na kukosekana kwa huduma ya
elimu kwa watoto katika kijiji hicho, hali hiyo imesababisha watoto wengi
kujiingiza katika vitendo visivyoendana na wao kama ndoa za utoto,mimba katika
umri mdogo na wizi kwa watoto wa kiume.
Sababu kubwa ya watoto wengi waliofikisha
umri wa kwenda shule kutokwenda ni umbali wa shule iliyopo katika kijiji mama
cha Fukayosi.
Ni takribani kilometa 12 huduma ya
elimu inapatikana hivyo kusababisha watoto kushindwa kwenda shule na kubaki
nyumbani na wazazi wao.
Watoto wengi walijaribu kwenda shule
lakini wameishia njiani kutokana na changamoto za umbali wa kilometa hizo
nyingi, huku wazazi wakiwa hawana uwezo wa kuwalipa gharama za usafiri wa
kwenda shule kila siku.
MADHARA YA BAADAYE
YA KUKOSA ELIMU
Subira Fikiri ni mtoto mwenye umri wa
miaka 15, anasema aliwahi kusoma shule ya awali kwa miaka minne baada ya kupona
akaamua kuacha na kubaki nyumbani na mama yake,hakuweza kwenda shule ya msingi
kwa sababu ya umbali.
“Nimebaki na mama yangu,baba
alishafariki nilipelekwa kusoma chekechea kwa miaka minne 20012-2015, kwani hii
ndio ipo hapa kijijini kwetu baada ya miaka yote nikaamua kuacha na sasa nakaa
tu nyumbani.
“Sijui kusoma wala kuandika kwani
nilishindwa kusoma shule ya msingi kwasababu ya umbali wa shule, hata
hivyo mama yangu hana uwezo wa kugharamia nauli hata uwezo wakunipangishia
chumba hana,”alisema Subira.
Subira ambaye tayari ana mtoto
aliyetimiza mwezi mmoja na siku 20, anasema amekata tamaa kabisa ya kupata
elimu kutokana na hali yake ya sasa.
“Baada ya kukaa nyumbani muda
mrefu sikuwa na la kufanya niliingia katika vishawishi vya kingono baada ya
hapo nikapata mimba na sasa nina mtoto mmoja katika umri huu mdogo sijui hata
nifanyeje,”anasimulia kwa masikitiko.
Kuhusu ndoto ya kupata elimu, Subira anasema
alitamani siku moja awe daktari ili aweze kuisaidia jamii ya Kitanzania.
“Ndoto yangu kielimu nilikuwa
nataka nisome ili niwe daktari nitibu watu hasa jamii yangu lakini sasa niko tu
hapa kijijini ndoto zangu, zimeishia njiani sasa nina mtoto ananitegemea, mama
yangu kama unvyomuona hana uwezo,nyumba yenyewe ndio hii inakaribia
kuanguka,”anaelezea Subira.
Subira anasema hata sasa anatamani
kusoma ili atimize malengo yake endapo kama atapata mtu wa kumsomesha.
“Natamani hata sasa
ningesoma,napenda kupata elimu, nikipata nafasi ya kusoma naamini nitafanya
vizuri na ninaweza kutimiza ndoto yangu,”anasema.
Mtoto mwingine, Salum Kindamba mwenye umri
wa miaka 14, licha ya umri wake wa kusoma kufika lakini bado hajaanza hata
darasa la kwanza na hajui kusoma wala kuandika.
“Wazazi wangu hawana uwezo wa
kumlipia nauli ya pikipiki ili niende shule hapa nina wadogo zangu watano wote
waliofikia umri wa kwenda shule hawaendi pia,naomba Serikali itujengee
shule,”anasema Kindamba.
Mmoja wa watoto anayesoma akitokea
kijijini hapo, Husen Saleh mwenye umri wa miaka 12 anasema anasoma darasa la
pili lakini kutokana na kuchelewa kufika shule imesababisha afanye vibaya
katika mitihani.
“Tuko wawili tu tunaokwenda
shule, tunapata shida ya usafiri wakati mwingine huwa tunaenda kwa miguu,wakati
mwingine tunavizia lift na wakati mwingine hatuendi kabisa shule.
“Tunaweza kufika darasani saa nne
au tano tukifika mwalimu ameshafundisha tunachukua madaftari ya wenzetu
tunaandika,mwalimu yeye hatuchapi kwasababu anajua tunatoka mbali lakini
darasani hatufanyi vizuri na hatusomi vizuri,”anaelezea Husen.
UMASKINI
UNACHELEWESHA UJENZI
Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kalimeni,
Amos Rungwa anasema usaili walioufanya Novemba mwaka jana watoto 120 wanatakiwa
waende shule.
Kwa mujibu wa Rungwa, eneo la ujenzi
wa shule tayari limeshatengwa na kupimwa hivyo kilichobaki ni ujenzi wa madarasa
kuanza.
“Takwimu za mwaka jana
tulivyoanza kupata kibali cha kuanzisha shule, tuna watoto wako mtaani 120
ambao wamefikisha umri wa kwenda shule ni miaka mitano sasa tangu kijiji
kimetenga eneo kwaajili ya ujenzi wa shule lakini mpaka sasa bado
hatujafanikisha.
“Tangu tumefanya takwimu wengine
wameshazaliwa na wengine muda wao wa kuanza shule umeshapita, mfano mtoto wa
miaka 7 anatakiwa aende shule sasa tunapobaki naye mpaka anafika miaka 14 hata
akipelekwa darasa la kwanza wenzake watamshangaa,”anasema Rungwa.
Anaeleza kuwa watoto wengi mpaka sasa
hawasomi na wako kijijini, huku wengine walioanza kusoma wakiishia katikati kwa
sasabu ya umbali wa shule kwani gharama za kupeleka mtoto shule nauli ya
pikipiki kila siku ni Sh 10,000.
“Wengi wako mitaani wengine
wameshaoa wengine wamepewa mimba wakiwa watoto,vijana wengine wamekuwa wezi
hata juzi tunatoka kuwafunga wawili miaka mitano mitano kwaajili ya wizi hali
hii inasikitisha,usafiri ni pikipiki ambapo gharama zake ni Sh 5000 kwenda na
Sh 5000 kurudi wazazi maisha duni hawamudu.
Anasema hali ya umasikni uliokithiri
katika kijiji hicho, unakwamisha kuanza ujenzi wa shule hiyo wanaendelea kuwahamasisha
wanakijiji waendelee kuchanga.
“Kama unavyoona ndugu mwandishi
hali ya hapa ni mbaya hata nyumba zetu unaziona hapa, wote masikini na darasa
moja linagharimu Sh milioni 15 huo uwezo wa kufikia hizo fedha ni ngumu ingawa
nitaendelea kuwahamasisha wanakijiji kuchanga na tumepanga kila kaya katika
kijiji watoe Sh 5000.
“Hivi karibuni tulipata barua
kutoka Ofisi ya Mratibu Elimu wa Kata ya Fukayosi ya kuanza kujenga shule
kuanzia la kwanza mpaka darasa la saba lakini bado hatujafanikisha zoezi la
uchangishaji.
Anawaomba wadau mbalimbali wa
maendeleo na Serikali,kujitokeza kuungana na wao katika kukamilisha ujenzi wa
shule hiyo ili watoto wapate elimu.
“Tunaomba wadau mbalimbali,
taasisi za kidini na Serikali waungane pamoja na sisi kuchangia gharama za
ujenzi wa shule ili watoto wetu wasiendelee kukaa mtaani na wao wanapata elimu
kama watoto wengine.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji
cha Fukayosi, Salum Mkecha anasema changamoto ya elimu ipo kwa vitongoji vyake
hasa Kalimeni ambayo ndio iko mbali zaidi kuliko vitongoji vingine.
“Vitongoji vinaumbali mrefu
kutoka kijiji mama cha Fukayosi tunaendelea kufanya juhudi ili shule hiyo
ijengwe,tunaendelea kuchangisha wanakijiji japo wana hali mbaya, tutajitahidi
kupita vitongoji vyote tisa kwaajili ya kupata mchango wa Sh
5000,”anaelezea Mkecha.
HALI YA HUDUMA
ZINGINE
Mwenyekiti huyo nasema hata huduma
zingine za afya,maji na barabara bado ni changamoto kwao.
Anasema katika kipindi cha mwaka 2008
na 2017 akina mama takribani sita walijifungulia barabarani, huku watu watatu
wakipoteza maisha kutokana na kukosa huduma ya uzazi.
“Ukiacha elimu hata huduma
zingine bado zinachangamoto kama huduma ya afya hatuna, hapa akinamama wakati
mwingine wanajifungulia njiani hata ukisema utakodisha gari barabara haipitiki.
“Hali hii imesababisha akinamama
kujifungulia barabarani kwamfano tangu mwaka 2008 hadi 2017, akinamama kama
sita wamejifungulia barabarani na pia watu watatu wamepoteza maisha mwaka 2017
mama na mtoto wote walipoteza maisha mwaka 2012 mtoto alipoteza maisha
kwasababu ya kukosa huduma,”anaelezea Rungwa.
Kwa mujibu wa Rungwa hata upatikanaji
wa maji katika kitongoji hicho ni changamoto kubwa.
Anasema maji yanaletwa kutoka sehemu
nyingine na wanalazimika kununua kwa dumu Sh 1500 hadi 2000 kwa dumu moja.
“Tulikuwa tumeshaanza kuletewa
huduma ya maji kwa mradi wa maji Wami Makurange tangu mwaka juzi, mipira
imechimbwa chini bomba ipo na tanki la maji lipo lakini hayatoi maji.
“Sisi tunategemea kuletewa dumu
ni Sh 1500 mpaka 2000 na sio watu wote wanamudu kununua maji kwa gharama hiyo
kubwa tunaomba Serikali pia iingilie hili maana hata mkandarasi wa mradi huu wa
maji hatumwelewi,”anabainisha Rungwa.
MBUNGE AAHIDI
KUTOA MATOFALI
Mbunge wa Bagamoyo, Dk.Shukuru
Kawambwa anakiri kuwepo kwa changamoto ya huduma za jamii katika kitongoji
hicho ikiwemo ile ya kupata elimu.
Anasema kutokana na hali ya umasikini
ya wananchi wake amechangia matofali 5,000, hivyo anaahidi kuwa atafuatilia suala
la ujenzi hadi utakapokamilika.
“Yote hayo nayajua na tunahangaikia
na tayari nimeshawachangia matofali,wananchi wangu ni masikini lakini nawaomba
waunge mkono juhudi za ujenzi wa shule.
“Nitaenda Kalimeni wiki ijayo
nijue wamefikia wapi na katika kikao changu nahamasisha sana hilo ni kweli
watoto kule hawasomi na sio jambo zuri pia naelewa umbali wa shule ni mrefu
nalifuatilia kwa ukaribu,”anaeleza Dk Kawambwa.
Dk. Kawambwa aliyepata kuwa Waziri wa
Elimu wakati wa Serikali ya awamu ya nne, anawaomba wadau wa maendeleo waweze
kuwasaidia ili kufanikisha huduma za jamii katika eneo hilo.
“Tunaomba wadau wa maendeleo
wajitokeze, ndugu mwandishi hata mimi nahangaika kuzungumza na wadau wengine
ili kufanikisha suala hilo la ujenzi wa shule,”anabainisha Dk. Kawambwa.
Kuhusu maji anasema yako katika hatua
ya kufika huko na muda sio mrefu watapata huduma hiyo na tayari mradi
umeshaanza.
Anasema pia atahakikisha barabara
inayoelekea katika kitongoji hicho itachongwa ili kurahisisha usafiri.
“Kuna mradi wa maji imeshaanza
kule hivyo wananchi wangu wasijali watapata maji na pia barabara inayoelekea
huko itachongwa ili iweze kupitika,”anaahidi Dk. Kawambwa.
UTARATIBU WA
SERIKALI
Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Zainabu
Kawawa anasema kwa utaratibu wa Serikali wananchi wanatakiwa waanze kujenga
baada ya hapo ndio wanaweza kupata msaada wa halmshauri.
Anasema hata hivyo baada ya kusikia
hali ya elimu atalifikisha suala hilo halmashauri.
“Kwa utaratibu wananchi
wanatakiwa kuanza wao wenyewe halafu halmashauri itawasaidi lakini kwasasabu
umeniambia nitalifikisaha suala hilo halmashauri,”anasema Kawawa.
↧
Bobi Wine: Tutaendelea kutetea haki ya wanyonge
Mahakama nchini Uganda imemfungulia mashtaka mbunge wa upinzani na mwanamuzi Muziki Robert Kyagulanyi maarufu kama Bobi Wine na watu wengine zaidi ya 20 kwa kumkasirisha rais Yoweri Museveni.
↧
Manara aburuzwa kortini, adaiwa Mil 83
HAJI Manara, Msemaji wa Klabu ya Simba na wenzake watatu, tarehe 6 Agosti 2019 wamefikishwa mahakamani kwa tuhuma za kudaiwa Sh. 83.5 milioni. Anaripoti Faki Sosi … (endelea). Msemaji huyo na wenzake (Beatrice Ndungu na Palm General Supply), wamefikisha kwenye Mahakama ya Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam wakidaiwa kupokea bidhaa zenye nembo ya Dela ...
↧
↧
Mchanga pekee ni kampeni ya mwaka mzima inayolenga kuhamasisha ukusanyaji wa chupa za plastiki na uhifadhi wa fukwe za bahari
MCHANGA PEKEE ni Kampeni ya miezi 12 iliyobuniwa, kuasisiwa na inayosimamiwa na Kampuni ya Coca-Cola Kwanza Kampuni Tanzu ya Coca-Cola Beverages Africa ikiwa imeanza mwezi Februari mwaka 2019 yenye malengo na madhumuni ya kuelimisha, kufundisha, kushirikisha na kuhimiza uhifadhi wa plastiki taka (mazingira) katika jamii zetu ikiwa imejikita katika usafishaji wa fukwe zetu, ukusanyaji wa chupa za plastiki, uchakataji na njia bora ya uhifadhi wa chupa za Plastiki nchini Tanzania.
↧
Familia yamrudisha Rooney England
Wayne Rooney amesema familia ndio imemuondoa DC United na kujiunga na Derby County.
↧
Tottenham Spurs yatupa kete yake kwa Dybala
Tottenham imekubali kutoa Pauni69 milioni kunasa saini ya mchezaji wa kimataifa wa Argentina Paulo Dybala majira ya kiangazi
↧
Zoezi La Utayari Kukabiliana Na Ugonjwa Wa Ebola Katika Wilaya Ya Buhigwe Mkoani Kigoma
Kufuatia nchi ya jirani (DRC) kuendelea kukabiliwa na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola tangu Agosti mwaka 2018. Serikali ya Tanzania imeendelea kuchukua tahadhari za ugonjwa huo kwa kupima utayari wa Watoa huduma za Afya kwa mikoa iliyomo hatarini kuathiriwa na ugonjwa huo.Serikali kupitia uratibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Menejimenti ya Maafa kwa kushirikiana na Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, pamoja na wadau wa maendeleo; WHO, FAO, USAID, HRH2030, na USAID Global Health Supply Chain Programu, inaendelea na zoezi la utayari wa kukabiliana na ugonjwa huo katika Wilaya za Mkoa wa Kigoma.Zoezi hilo linalenga kuwaimarisha watumishi hao katika maeneo maalum ikiwemo ya uratibu, utambuzi na ufuatiliaji wa wagonjwa iwapo atagundulika, matibabu ya wagonjwa, uchukuaji na usafirishaji wa sampuli na kuthibitisha maabukizi pamoja kuimarisha mifumo ya utambuzi wa masuala ya Afya kwa kila abiria wanaopita kwenye mipaka ya mkoa wa Kigoma.
↧
↧
Edouard Mendy: Senegal goalkeeper ready for Rennes adventure
Senegal goalkeeper Edouard Mendy is ready for a new adventure at French Ligue 1 club Rennes after joining from rivals Reims.
↧
Brazil: Amazon deforestation rises rapidly
A government institute at loggerheads with Brazil's President Jair Bolsonaro has called the massive increase a "major setback." The right-wing administration's pro-agrobusiness policies are to blame, the agency claims.
↧
Mfungwa aliyevaa nguo za kike ili atoroke jela ajinyonga
Mfungwa wa dawa za kulevya ambaye alikamatwa baada ya kujaribu kutoroka gerezani akiwa amevalia nguo za kike amefariki dunia.
↧
Lowry atoboa siri ya Leonard kuondoka Toronto
Mlinzi wa timu ya Marekani ‘All Star’, Kyle Lowry amesema anajua kwanini Kawhi Leonard angeondoka kwenda Los Angeles Clippers, lakini kiongozi huyo wa muda mrefu wa Toronto Raptors hana mpango kuondoka Canada.
↧
↧
Bolton: US Ready to Sanction Those Who Do Business with Maduro Government
One day after the U.S. imposed a full economic embargo on Venezuela, National Security Advisor John Bolton says the U.S. can now sanction anyone who supports the government of President Nicolas Maduro. Maduro’s government denounced the sanctions as a "grave aggression" that will lead to "the failure of political dialogue." VOA’s Diplomatic Correspondent Cindy Saine has more from the State Department.
↧
Volatility, Uncertainty as US-China Trade War Escalates
U.S. financial markets struggled to rebound Tuesday after their biggest drop since December. U.S. President Donald Trump’s top economic adviser says the White House has the upper hand in deepening trade and monetary disputes with China -- an assertion made after Beijing announced it will no longer buy U.S. agricultural products. VOA’s Arash Arabasadi reports.
↧
Jumping Like a Lemur, Flying Like a Dragonfly – Robots That Mimic Animal Movements May Be On Their Way
In a laboratory in California, engineers are working on pushing the boundaries of how robots move, imitating the ways some animals jump, fly or crawl. Michelle Quinn met Salto, a one-legged jumping robot to see the future of robots.
↧